Mtandao wa
Asasi za Kiraia Wilayani Bagamoyo (BANGONET) umeomba serikali kutumia ruzuku ya
mfuko wa jimbo kuchapisha na kusambaza katiba kwa wananchi ili waweze kusoma na
kuielewa kabla ya mchakato wa kutoa maoni.
Ombi hilo
limekuja baada ya kufanya mdahalo na wananchi katika majimbo ya Bagamoyo mjini
Chalinze ambayo ilihudhuriwa na wananchi 473 ambapo iligundulika kuwa ni
wananchi wachache takribani asilimia 10 kati ya asilimia 100 ndio wanaitambua
katiba na kati ya hao asilimia 5 tu ndio wamewahi kuisoma katiba ya sasa.
Akizungumza na
waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jana Katibu
Mtendaji wa Asasi hiyo Leonard Bamkuwia alisema Katiba zinapatikana katika duka
la serikali lililopo Dar es Salaam kwa bei ya shilingi 5000 kila nakala 1 bei
ambayo mwananchi wa kawaida hawawezi kuimudu na si rahisi kufika jijini Dar es
Salaam kwa ajili ya kutafuta katiba
“Ili
kuwawezesha wananchi kushiriki katika kutoa maoni yao juu ya kuandika katiba
mpya ni vema serikali ikachukua jukumu la kuchapisha nakala za katiba na
kuzisambaza kwa wananchi mijini na vijijini,”.
Alifafanua
kuwa mjadala ambao umekuwa ukiendelea Bungeni kuhusiana na katiba mpya
ulitawaliwa na misingi ya kibinafsi na ushabiki wa vyama vya kisiasa pasipo
kuzingatia masuala ya kitaifa.
Bamkuwia
alisema maadili ya kitaifa na uzalendo vimetoweka na hivyo kuwa na matabaka ya
walio nacho na wasionacho ambavyo vimepelekea watanzania kuitwa mafisadi,
kukithiri kwa vitendo vya rushwa na mawaziri kuingiza wananchi katika mikataba
mibovu isiyokuwa na maslahi ya kitaifa.
Pia,
alisisitiza kuwa na sera au mfumo wan chi unaoeleweka na utakaofuatwa na marais
wote bila kujali itikadi za vyama vyao wanavyotoka.
No comments:
Post a Comment