TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Tuesday 22 May 2012

Keisha aitaka jamii kusaidia walemavu wa ngozi

 MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Khadija Shabani ‘Keisha’ ameitaka jamii kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) katika sekta mbalimbali ikiwemo pesa za kununulia mafuta ya kupunguza vidonda na muwasho wa ngozi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Keisha alisema walemavu wa ngozi  wanakumbana na changamoto nyingi ikiwemo kuishi kwa wasiwasi kutokana na watu wenye imani za kishirikina kudhani kwamba ngozi hiyo ni chachu ya kujipatia utajiri.

Alisema hata yeye amewahi kukabiliwa na changamoto nyingi katika maisha yake kutokana na hali ya kuwa na ulemavu wa ngozi, hivyo ameitaka jamii kuwasaidia albino katika elimu, ajira na kuwalinda dhidi ya wauaji.

Alisema vitendo vya unyanyasaji dhidi yao vinazidi kuongezeka, licha ya serikali kudhibiti na kufanikisha azma yao na baadhi ya watu wenye imani hizo walifikishwa mahakamani na kuchukuliwa hatua.

“Mwanzo, vyombo vya dola vililishughulikia jambo hili na kulidhibiti kwa kiasi kikubwa lakini kwa sasa linajirudia na linazidi kuongezeka siku hadi siku na serikali inashindwa kuchukua hatua kama zile za awali” alisema Keisha.

Akizungumzia maisha yake ya awali alisema aliwahikuchukizwa alipokuwa mtoto kutokana na baadhia ya watoto kumuita ‘Zeruzeru’ na alijiona kama si mmoja kati ya watoto hao hadi kufikia hatua ya kumwambia mama yake hataki kwenda shule.

No comments:

Post a Comment