BAADA ya kutamba na wimbo wake wa ‘Mi sio sharobaro’, msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Alli
Momba 'Momba' anajipanga kuachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina
la ‘Mdundiko’ ambao amemshirikisha nyota wa muziki huo, Juma Kassimu
'Juma Nature'.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Momba alisema wimbo huo
unatarajiwa kuwa tofauti na nyimbo nyingine alizowahi kuzifanya.
"Nimefanya
vizuri sana katika wimbo huo kutokana na ubunifu ambao nimeufanya hali
inayoashiria naweza kumfunika Juma Nature ambaye nimemshirikisha katika
singo hiyo," alisema Momba.
Pia, msanii
huyo aliwaomba mashabiki wa muziki huo kumpa ushirikiano wa kutosha
katika wimbo anaotarajia kuuachia wakati wowote kuanzia sasa, pamoja na
kazi zake zijazo.
Mbali
na kujiandaa kutaka kutoka na kibao hicho, Momba alishawahi tamba na
vibao vyake kama vile Nikusabahi, Kabwela, ambavyo vilifanya vizuri na
kumtambulisha katika tasnia hiyo.
No comments:
Post a Comment