Rais
wa Marekani Barack Obama anaunga mkono moja kwa
moja ndoa za watu wa jinsia moja, akiwa
rais wa kwanza kufanya hivyo nchini humo.
Obama
amesema kuwa alisita, kwa sehemu, kuhusu ndoa za
watu wa jinsia moja kwasababu alifikiri kuwa
mahusiano ya watu wawili kwa mujibu wa sheria za kiraia yanatosha.
Katika mahojiano ya
televisheni katika ikulu ya Marekani ameeleza kuwa
alikuwa na shaka kuhusiana na ukweli kwamba
watu wengi neno ndoa ni jambo ambalo
linazusha hisia kali za kitamaduni na
imani za kidini.
Obama amesema kuwa kwa
sasa ni muhimu kwake binafsi kujitokeza na
kuthibitisha kuwa mahusiano ya watu wa
jinsia moja yanafaa kufikia kuwa watu hao
wanaweza kuoana.
Source: Dw
No comments:
Post a Comment