Na Mwandishi wetu
Kituo cha Utoaji Taarifa (TCIB)
kimetoa hati ya uchaguzi huru na haki kwa asilimia 70 kwa Tume ya Uchaguzi nchini kutokana kufanikiwa kusimamia uchaguzi
kwa uhuru, amani na haki katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni katika jimbo
la Arumeru Mashariki .
Wakizungumza na waandishi wa Habari
viongozi wa Kituo hicho walisema wametoa asilimia 70 kwa tume hiyo pia kutokana
na kuboresha baadhi ya mapungufu yake ikiwemo ni pamoja na maboresho ya mfumo
wa daftari la kudumu la wapiga kura.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho
Deus Kibamba alisema Tume ya uchaguzi imefanya maboresho katika daftari la
kupiga kura nab ado imeonyesha mipango yake ya kuboresha ambayo itatangaza siku
za karibuni.
Pamoja na hati hiyo, kuna mapungufu
ambayo wameyaeleza kwamba yametokea wakati uchaguzi unafanyika kuwa ni pamoja
na rushwa, vitisho kwa viongozi wa kisiasa na
lugha za matusi.
Akizungumzia mapungufu hayo Afisa
Tawala wa Kituo hicho Debora Mushi alisema wakati wa uchaguzi kulikuwa na
magari yanayokimbizana ili kutoa rushwa hivyo kuitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) kuwajibika ipasavyo dhidi ya watu hao.
Pia, alisema kuna baadhi ya boda
boda zilikuwa zinafuata msafara wa wanasiasa lakini jambo la kushangaza
walikuwa wakifika eneo la tukio wanadai fedha kitu ambacho kilikuwa sio sahihi
kwasababu hawakulazimishwa kujiunga kwenye msafara.
Vile vile, alisema lugha ya matusi
ilikuwa ikitumiwa na wagombea wa vyama nane ambavyo vilikuwa vikipiga kampeni,
kwani badala ya kuzungumzia changamoto zinazoikabili Arumeru wanazungumza
matusi kwa wananchi hivyo wanahitaji kuwajibishwa.
No comments:
Post a Comment