NYOTA
wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ally Timbulo kaachia wimbo wake mpya
unaokwenda kwa jina la ‘Samson na Delila ambao umezungumzia zaidi mapenzi na jinsi
ambavyo mwanamke ana nguvu katika ushawishi wa mapenzi.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam jana, Timbulo alisema wimbo huo katengeneza tofauti na
nyimbo zake nyingine kwa lengo la kuwapa ladha tofauti mashabiki wake.
“Wimbo
huu naamini utafanya vizuri zaidi na mashabiki wangu wataupenda kupita kiasi
hivyo nawaomba wapenzi wangu waeendelee kunipa sapoti katika kazi zangu”
alisema Timbulo.
Alisema
wimbo huo uko tofauti na nyimbo zake ambazo zimewahi kutamba kwani amewaletea
mashabiki ujumbe ambao ameuandika yeye mwenyewe tofauti na zile za mwanzo
ambapo ilisemekana ameiba kopi kutoka kwa msanii wa Cameroon wanaojulikana kama
X Maleya na wimbo wao unaoiywa yelele
Mbali
na wimbo huo, Timbulo alishawahi tamba na nyimbo zake kama Domo langu, na ‘wa
leo wa kesho’ nyimbo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika vituo
mbalimbali vya redio na luninga.
Msanii
huyo amewaahidi mashabiki wake kwamba kwa sasa atawaletea nyimbo ambazo sio za
kopi tena kwani amejipanga mwaka huu kuwaletea nyimbo ambazo ni nzuri na
zitakazowafurahisha.
No comments:
Post a Comment