Katibu Mkuu wa Umoja
wa Mataifa, Ban Ki Moon, amemteua Naibu Katibu Mkuu anayemaliza muda wake Dkt.
Asha-Rose Migiro kuwa mjumbe wake maalum katika masuala ya Ukimwi na ugonjwa wa
Ukimwi Barani Afrika.
Katibu Mkuu Bw. Ban Ki
Moon ameeleza kwamba ingawa Migiro alikuwa naibu katibu mkuu wake lakini
amekuwa mwalimu wake na amejifunza mengi toka kwake na daima ataendelea kuenzi
mchango wake mkubwa.
Amemuelezea Migiro
kama kiongozi si tu mwadilifu, lakini mwanadiplomasia aliyebobea, aliyefanya
kazi kubwa, ngumu na nzito kwa moyo mkunjufu, uhodari , umakini, na uadilifu wa
hali ya juu sana.
Source. Mo blog
No comments:
Post a Comment