Viongozi wa Kiislam nchini Kenya
wamekubaliana kuunda vikundi binafsi vya ulinzi ili kulinda makanisa kufuatia
kushambuliwa siku ya Jumapili.
Kufuatia mashambulizi hayo watu 15
waliuawa katika upekuzi wa makanisa Garissa katika mji ulio karibu na Somalia.
Mipaka ya Kenya imekuwa sio salama
tangu ilipotuma askari wake kwenda Somalia kupambana na kikundi cha kiislam la
Al Shabaab
Adan Wachu ambaye ni kiongozi wa
Baraza Kuu la Kiislam nchini Kenya aliiambia BBC kuwa uvamizi huo ni kitendo
cha kigaidi.
"Kuna watu pale wanaotaka
kuifanya Kenya kuwa kama Nigeria nyingine,” alisema Wachu
No comments:
Post a Comment