TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Monday 6 August 2012

Dongo Janja ameachia ngoma yake mpya


Msanii wa bongo fleva nchini Abdul Chende ‘Dogo Janja, ameachia kibao chake kipya kinachoitwa natoa ya moyoni ikiwa ni rekodi yake ya kwanza  chini ya usimamizi wa Ustadh Juma mwenye kundi la Mtanashati ambaye alimchukua kukiendeleza kipaji chake.

Dogo Janja ambaye awali alikuwa akifanya kazi na Kundi la Madee, alisema kibao hicho amemshirikisha PMC na amerekodi kwa Michael Chali .

Alisema “Nashukuru Mungu mtanashati wamenisaidia nimerekodi wimbo kwani kuna watu walidhani kwamba siwezi tena kuendelea kuimba lakini Mungu yupo pamoja name, ninaendelea kama kawa,”

Msanii huyo alikwaruzana na Madee siku za karibuni, na hivyo kurudishwa kwao Arusha, ambapo Mtanashati aliona amchukue ili kipaji chake kisipotee.

Dogo Janja alisema hana kinyongo na Madee na anashukuru kwa kumfanya ajulikane kwa vile kama sio yeye pengine asingejulikana, lakini zaidi alimshukuru Tunda man kwa kutoonyesha kinyongo kwake.

No comments:

Post a Comment