Na Rushyd Ahmed
SERIKALI ya Zanzibar inakusudia
kuanzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji. Waziri wa Maji, Ardhi,
Makazi na Nishati, Ramadhani Abdallah Shaaban, ameliambia Baraza la
Wawakilishi.
Waziri alitoa kauli hiyo wakati
akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara yake kwa mwaka wa
fedha 2012/13 katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kin…achoendelea
Chukwani, Zanzibar.
Alisema tayari mataarisho ya
Sheria ya kuanzisha Chombo hicho yameanza, sambamba na Sheria za
kusimamia na kusambaza nishati ya mafuta na Petrol ya Zanzibar.
“Mheshimiwa Spika kwa ajili ya
kutekeleza sera ya Nishati Zanzibar, Wizara inaendelea kujiandaa pamoja
na kuwapatia mafunzo wafanyakazi katika sekta ya nishati na mafuta,”
alisema Waziri Shabaan.
Alisema juhudi za kuwapatia
mafunzo wafanyakazi wa Wizara hiyo zinalenga kukabiliana na upungufu wa
wataalumu wa fani ya nishati ikiwemo kutafuta na kuchimba mafuta katika
Visiwa vya Zanzibar.
Aidha, alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Serikali ya Norway inafanya mpango wa kufanya semina na kongamano kwa lengo la kutoa taaluma kuhusu athari za kimazingira zinazotokana na kutafuta na kuchimba mafuta Zanzibar.
Kuhusu tathmini ya kimazingira
inayotokana na mwelekeo wa kutafuta na kuchimba Mafuta na Gesi asilia,
Waziri alisema Wananchi katika Visiwa hivyo wamekuwa na matumaini
makubwa ya kuwepo kwa nishati hizo.
Waziri Shabaan, alisema katika
mwaka wa fedha unaoanza, Wizara yake pia imepanga malengo ya kuendelea
na juhudi za kuwapatia wananchi wa Zanzibar elimu juu ya matumizi ya
nishati.
SOURCE: Swahili Villa
No comments:
Post a Comment