Mimi
kama Mtanzania nadhani sasa Dini zinavuka mipaka kuingilia Serekali na sheria
za nchi. Serekali iliyopo madarakani iliekwa na Watanzania kwa kupiga kura Kikatiba
na Rais akapatikana na akaapishwa kuiongoza Tanzania kwa ridhaa ya Watanzania.
Kitendo cha Rais kuapishwa ni kwamba hata mwenyezi Mungu amebariki uteuzi wake na
kuikubali Serekali iliyopo madarakani.
Kinachonishangaza
ni kuona Dini sasa zinavunja Katiba ya nchi na sheria za nchi kwa kuingilia
majukumu ya Serekali na Mahakama ambazo kikatiba ndizo zinatoa haki kwa kila
mtu. Haki ya kisheria za uhalifu haitolewi Makanisani wala Misikitini. Mhalifu
anapofanya makosa ya jinai au uhalifu wa aina yoyote ile haki yake inapatikana
Mahakamani na sio Kanisani wala Misikitini.
Watu
wanaolalamika kuwa Mtoto kakojolea Msahafu walikuwepo wakati kitendo
kinafanyika na hawakuchukua hatua yoyote kufanya vikao vya pamoja kufanya
maamuzi yaliyo sahihi kulingana na sheria za Dini wala Sheria za Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wakati watu wanajichukulia sheria mikononi mwao kuchoma Makanisa na kuharibu mali za watu sikuona Mzee wa Kanisa, Shehe wa
Msikiti, wala Mkuu wa Wilaya wala Mkuu wa Mkoa aliyetoka kuwaomba vijana
wasiharibu mali.
Wengi wa watu hawa walikaa majumbani mwao kuangalia Television huku wengine
wakicheka na kushangilia na Wangine wakilia na kusononeka. Mimi nawajua
wanadamu ndivyo ilivyokuwa siku hiyo.
Mimi
nilichoona ni Jeshi la Polisi kuingilia kati sakata hilo na kufanikia kuzima
vurugu hizo kwa maana hiyo Jeshi la Polisi liliona ni jukumu lake kuingilia
kati uvunjifu huo wa amani na uharibifu wa mali za Watanzania waliojinyima
kuzitafuta ili kujiendeleza na kuipatia Serekali kipato. Hili ni kosa la jinai
kisheria na Watanzania wanatakiwa wawe watulivu wakati Serekali na Mahakama zinafanya
kazi yake Kikatiba ya kutoa maamuzi. Endapo Kanisa au Msikiti utakuwa
unaingilia sheria za nchi mimi sioni sababu ya kuwa na Serekali, Katiba, Sheria
na Mahakama. Hivyo naiomba Serekali hivi vikao vinavyofanyoka sasa katika
Makanisa yetu na misikiti kuzungumzia watu waliopo chini ya mikono ya Serekali,
chini ya mikono ya Sheria wachunguzwe na waunganishwe kwenye makosa yale
yaliyotokea. Ilianza hivyo kidogo kidogo ndio ukatokea uvunjifu wa amani.
Serekali ya mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete itafute mda ikae na wakuu wote wa
Serekali za Wilaya, Mikoa, wakuu wa Misikiti, na Makanisa kuinya hilo. Ili
kesho hivyo vikao hivyo vya usiku visije kutuletea balaa. Hakuna mtu yuko juu
ya Serekali, Katiba ya nchi na Sheria za nchi. Hivyo vikao vya usiku vya kutetea
wahalifu ni uhalifu vile vile. Kwa hili naomba Serekali na Jeshi la Polisi
wajipange. Usipoziba ufa
utajenga ukuta.
Katiba
ya nchi inaeleweka, na Sheria za nchi pia zinaeleweka. Anayefanya maamuzi ya
kesi zote za jinai na uhalifu wa aina yoyote ile ni mahakama na sio Kanisa wala
Misikiti. Mimi nawashauri watu wanaojaribu kuingilia mihimili ya sheria za nchi
wachukuliwe hatua za haraka sana
bila kujali Dini zao. Nchi inaendeshwa na utawala washeria na sio Makanisa na Misikiti.
Kila muumini najua Sheria za nchi na sheria za Dini yake. Kama
wewe ukijaribu kuvunja Katiba ya nchi na sheria za nchi kwa kutegemea kuwa
Waislamu au Wakristo wataandamana ili utoke imekula kwako. Hatutavumilia nchi
iingie kwenye vurugu za kidini na machafuko eti kwa kuwa Mkristo au Muislamu
kawekwa rumande kwa ama kuua, kuharibu mali, kukashifu Serekali au
vinginevyo.
Kwa
hili naishauri Serekali ikae na hawa wakuu wote wa Dini na kuweka bayana kwao
kuwa Serekali na Sheria za nchi ni namba moja Dini inafuatia. Kama
hakuna Serekali na sheria nchi haitatawalika. Serekali ikiruhusu kila mtu, kila
Dini au kila muumini kufanya maamuzi yake hii nchi itakuwa Somalia. Mwisho
naiomba Serekali ichangie kwa hali na mali kujenga Miundo mbinu, Makanisa,
Misikiti, na kila eneo lililoharibiwa na vijana wetu kwani sisi ndio
tunachelewa kutoa somo la malezi kwa jamii. Kama Makanisa na Misikiti
haitakuwepo tutaanzisha vijiwe haramu. Sisi ndio tunalea uozo katika familia
zetu. Serekali ikichangia ni kila Mtanzania atakuwa amechangia hivyo kila mtu
itamuuma na sio rahisi tena Wazazi kuruhusu au kuachia watoto kuwa waharibifu.
Mimi narudia tena kwa hili la vikao vya usiku vya kuijadili Serekali, Katiba ya
nchi, na Sheria za nchi IGP Mwema usicheke nao watakupaka kinyesi. Wewe ni
Kamanda uliyepewa rungu la kuchunga Raia na mali zao usifanye masihara. Kila
anayevunja Katiba na Sheria za nchi lazima aende lupango, hakuna cha mototo wa
Tumboni wala Mgongoni. “MCHELEA MWANA KULIA HULIA YEYE”
Mkereketwa.
Lengai
Ole Letipipi
No comments:
Post a Comment