Wakati
Watanzania tuko kwenye maandalizi ya kutunga katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania bado mimi nasisitiza sheria za nchi ziboreshwe kwani limezuka wimbi
la watu kutokuogopa wala kujali sheria. Mumejionea wenyewe mambo wanayofanya
hawa binadamu.
Kuna baadhi ya matukio ya hivi karibuni
yanathihirisha kuwa bado kuna haja ya kuwafanya binadamu waogope kutenda maovu.
Adhabu kama za kifungo cha miaka 30 au kifungo cha maisha bado ni adhabu ndogo
sana.
Mtu anayetaka eti kuingia Ikulu kwenda kumuona Rais wakati amebeba mawe au
panga na yuko Waziri mwenye mamlaka hataki kwenda kumuona huyu kifungo chake ni
Maisha na ikidhihirika dhana yake ni kumdhuru Rais tena wa Jamhuri huyu anyongwe
hadi kufa.
Wanataka kutuingiza kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe hawa.
Anyongwe hadi kufa. Rais ndiye anatakiwa kutangaza hali ya hatari wewe
unatangaza kama nani wewe kikaragosi. Alafu unakimbilia Ikulu mwenyewe hata
hayupo. Hawa ndio wabakaji, wezi, wachawi, wala unga, wavuta bangi, wanywa
gongo. Sitaki kusikia habari zao wapewe adhabu kali sana. Manaenda Ikulu
tumewapigia kura za ndio.
Kwa kuwa Rais ni mtu aliyepewa madaraka na
Watanzania awe kwa kushinda kura au kwa kuchakachua lakini akishakuapishwa kuwa
ni Rais hakuna tena mambo ya kusema kaiba kura.
Huyu lazima tumpe heshima zake.
Sasa wavuta bangi, wanywa gongo, na wabuya unga wanajikusanya tu na kudai
wanataka kwenda Ikulu kumuona Rais mimi nadhani sio sawa. Hawa watu wanataka
kuleta uvunjifu wa amani kwani Rais akipata matatizo nchi nayo inaingia kwenye
matatizo bila kujali huyu ni CCM, CUF, CHADEMA, NCCR, SAU, au TLP. Hawa wakora
waliotaka kwenda Ikulu wapewe adhabu kali sana kila mtu ajue kuna Serekali.
Mwisho
vitendo vya watu kuchukua sheria mikononi na kuanza kuashibu wenzao kwa kuchoma
makanisa na misikiti iliyojengwa kwa gharama mimi naona adhabu yake ni kifungo
cha maisha au kunyogwa. Hatuwezi vumilia watu wanaleta tabia za udini udini
ndani ya nchi wanaangaliwa tu kama vile hakuna sheria. Hii ni kunyima haki za
watu wengine za kuabudu dini wanazotaka.
Mtoto wa miaka 14 bado no mdogo sana
kujua athari za kukojolea msaafu. Huyu adhabu yake ni bakora tu. Unachoma Kanisa
kwa ajili ya motto kama huyu na hata historia yake hauijui. Hawa wote
waliohusika adhabu yao kifungo cha maisha au kuntogwa labda tu wawe wana umri
chini ya miaka 18 ndio sheria ziangalie adhabu inayowastahiki.
Kiongozi yeyote ndani ya nchi anayesababisha
mikusanyiko ya dini au ya Siasa isiyo halali lazima sheria ichukue mkondo wake.
Mimi nasisitiza hilo kwani kuna watu wanajifanya wanamjua Mungu kuliko wenzao.
Kila mtu anajua Mungu yupo ni yuko hai na anaishi, na ataishi milele na milele.
Lakini huwezi kuwashurutisha wenzako kuchoma Makanisa au Misikiti kwa
visingizio, eti huyu kakojolea Msaafu, eti oh Yesu sio Mungu wewe inakuhusu nini
kama Yesu sio Mungu.
Fuata Mchungaji wako au Shehe wako anakufunza nini katika
imani yako ya Dini. Majigambo, Masifa na mabishano barabarani sio kuwa mcha
Mungu. Umesikia watu wanabishania Dini wewe kimbilia Biblia yako au Msaafu wako
soma kila mstari unaozungumzia hayo mabishano utapata jibu.
Mwisho namuomba mheshimiwa Rais akubali kuweka
saini kwenye karatasi anazoletwewa na Majaji zenye adhabu ya kifo. Watu tumekuwa
wakaidi. Bila adhabu kali kuwepo kwenye katiba ya Jamhuri utawakuta watu wako
Ikulu wanataka nao wale na Mheshimiwa au walale Kitanda cha mheshimiwa huu ni
ukora lazima tuukomeshe. Wanyongwe hadi kufa.
Mkereketwa
Lengai Ole
Letipipi.
|
Thursday 25 October 2012
Sheria za Tanzania ziboreshwe
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment