TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Wednesday 31 October 2012

Tuna bahati na rasilimali lakini hatuna bahati na viongozi

Tanzania tumebahatika kuwa na rasilimali za kila aina ikiwepo madini, wanyama, ndege, bahari, maziwa, malima, ardhi, misitu na kadhalika lakini Mwenyezi Mungu akatunyima viongozi bora.

Toka afariki Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere tumekuwa yatima kama Watoto wa vifaranga ambavyo Mama yao amechukuliwa na mwewe. Watanzania hatuna haki katika nchi yetu. Viwanda wameua, Viwanja vya wazi wamegawana, Mashamba ya Serekali wamegawana. Nchi imekuwa mufilisi. Mimi hata sioni sababu ya kuzungusha Mwenge wa Uhuru. Hiyo fedha wapeni watoto yatima na wajane mtapata fadhila.

Viongozi wanasimama majukwaani kutangaza sera nzuri sana mbele ya watu waliowapigia kura lakini wakishafika maofisini ni kama wamelogwa. Hebu shuhudieni haya hapa chini.

-Kiongozi anakaribisha Wawekezaji kwenye sekta ya madini lakini nchi inaambulia asilimia tatu tu ya madini yanayochibwa nchini.

Serekali imekuwa sio sikivu tena Viongozi wamekuwa wafanya biashara. Watu wanafanya biashara Ikulu. Nani asiyejua kuwa Ikulu imekuwa ya biashara. Nani asiyejua kuwa karibuni miradi yote ya wawekezaji nchini wako viongozi wakubwa ndani. Nani asiyejua kuwa viongozi wetu waliviua viwanda vya ndani ili wafanye biashara. 

Kama sivyo kulikuwa na haja gani kukiua kiwanda cha Matairi kule Arusha na kila siku Watanzania wananunua magari. Mimi nasema lazima tujaribu watu wengine CCM sasa basi. Wameweka watoto wao madarakani ili kuitawala Tanzania kama Koloni lao. Aliyeishitaki Serekali ya CCM kwenye mahakama ya Kimataifa alifanya vizuri sana na nampa heko. Wakitaka ushahidi walete waonyeshe mashule wanayosoma watoto masikini, waomyeshe zahanati zetu, waonyeshe viwanda walivyoua, waonyeshe makaburi ya Alibino na makaburi ya watu waliouwawa na Polisi. Wakitaka ushahidi zaidi tupo Watanzania ambao tutatoa ushahidi mpaka wa Mali zao wanazomoliki.


-Kiongozi anapita kuwaomba Watanzania kura za ndio lakini akishazipata anatuma watu kuwavunjia watu hao hao makazi yao.

Kinachofanyika sasa hivi Tanzania ni ukora na uonevu kwa watu wanyonge. Mimi naishangaa Serekali sikivu kwa kuomba kura za ndio lakini watu wanapovunjiwa nyumba zao na kulala na familia nje haiwakeri. Nawashangaa Watanzania kuikumbatia Serekali sikivu saaa ya uchaguzi lakini uchaguzi ukipita wanalia na kusaga meno. Maisha imekuwa magumu sana kiasi kwamba mtu anayepata mlo mmoja kwa siku anashukuru Mungu. Wengi wa Watanzania sasa hivi hawali wanashinda njaa kutokana na ukame lakini Serekali sikivu ipo. Serekali sikivu wananchi wanalala nje. Serekali sikivu watu wake wanapigwa risasi hovyo. Ameuwawa Mwangosi hamkutoka maofisini. Ameuwawa Askari tena labda kwa bahati mbaya au labda kwa kugombania wanawake watu wote wametoka maofisini. Kamanda wetu kauwawa kwa bahati mbaya tu, mbona Mwangosi aliuwawa kwa makusudi lakini hata tume mliyounda wenyewe imepindisha maelezo. Tunaomba watu zaidi wajitokeze kuishitaki Serekali ya CCM kwenye mahakama ya Kimataifa. Wanazo kesi za kujibu. Kama hawana kesi za kujibu kwa nini Waziri mkuu alilia ndani ya Bunge.

-Kiongozi anatumia mabilioni kutangaza utalii ili watu waje kwa wingi wakati huo huo anaongeza bei za kuingia kwenye hifadhi wakati huo huo anafanya biashara ya kuuza wanyama na ndege.

Mimi huwa naishangaa Tanzania sio bure Kadfa wa CCM ndugu Kusila akasema Tanzania inapelekwa Mochwari. Hivi kama unauza Wanyama na ndege nje ya nchi maana yake si hao watu wanaenda fungua hifadhi zao za ndani. Sidhani kuwa wanaenda kuwala. Kama wanaenda fungua Zoo za kuweka wanyama maana yake si kwamba wanapunguza idadi ya Watalii kuja Tanzania. Tunaona ugumu gani kuwachinjia watoto wa shule nyumbu wakala kuongeza virutubisho mwilini kuliko kuwauzia Watu wakafungua Hifidhi zao za wanyama ndani. Ukimuuza mnyama na ndege wako huku unapandisha bei za kutembelea hifadhi matarajio yako ni nini hasa. Watu wanachimba madini ndani ya hifadhi za Taifa kule Serengeti mpaka Watanzania wananyimwa kupita na watalii maeneo hayo. Watu wanaporwa aedhi yao kwa ajili ya wawekezaji. Mimi napenda tu hata hao wanaosaidiwa kupora wajue Tanzania ni ya Watanzania na sio ya mtu wa kuja. Kama waliweza Wazimbabwe kuwatoa wawekezaji sisi Watanzania tutashindwaje?. Kilichonishangaza zaidi ni kuingilia hata ardhi yetu Masaini kule Ngorongoro. Jiandaeni sana lakini niwajulishe tu kuwa La Mgambo limelia na likilia kuna jambo!

Mkereketwa!
Lengai Ole Letipipi

No comments:

Post a Comment