TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Tuesday 6 November 2012

Asemavyo mkereketwa kuhusu ujenzi wa barabara

Mimi sidhani maisha bora yanaletwa na kujenga barabara na wala sidhani kutembea sana Duniani ndio maendeleo. Kagame, Mwai Kibaki, Museven, Mugabe wameenda mara ya mwisho Ulaya lini mbona wanayo maendeleo. Wala Tanzania mbele ya Wakenya, na Wanyarwanda tusiongee kitu kabisa.
 
Sisi tutaendelea kudangaywa na Siasa mpaka mwaka 2015 tutwapigia tena kura. Maendeleo ya Barabara huku watu wako hawajui kusoma na kuandika ni maendeleo gani?. Maendeleo ya Barabara huku watu wako hawana ajira ni maendeleo gani?. Kwani Barabara zikiwa za vumbi lakini Watoto wanaomaliza shule wanakuta viwanda kede kede na kupata ajira kuna shida gani?. Barabara Tanzania safi lakini afya za watumiaji matatani, hoi bin taabani. Elimu ndio usiseme.
Kama ni mimi Rais Jakaya Mrisho namfukuza kazi Magufuli kwa kunikejeli. Yani Watanzania wote wanalalama kuwa Safari za mheshimiwa zimezidi na zinatia hasara yeye anasema zinaleta maisha bora kwa kila Mtanzania. Tumefaidika nini na safari zake wakati nchi inadaiwa trilioni 22. Miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika watoto wanakaa chini wakiandika, Hakuna Zahati wala Madawa ya Tiba, Wanafunzi wanamaliza shule hakuna ajira viwanda vyote kwishnei, alafu mnasema kusafiri ndio maendeleo.
 
 Watanzania wanakaa nyumba za tembe nyie mnajenga mabarabara mpitishe malori yenu kwendeni zenu huko. Kwani hatujui Ridhiwani ndiye anajengewa barabara malori yake ya mafuta yasimwingize gharama za kununua spea. Nani mjinga Tanzania hii siku hizi.
Au maendeleo ni kuficha fedha Ulaya, au Kuuza meno ya Tembo, au kuuza Wanyama, na kufanya biashara ya kuuza watu kama sasa zinavyofanyika. Au Watanzania hamjui Tanzania kuna biashara ya utumwa. Kule Arusha kuna Tajiri anaitwa Salum Ally yuko rumande kisa amewarusha wakubwa kwenye biashara ya kuuza watu.
 
 Wamefanya naye Biashara ilivyofika uchaguzi alivyokataa kumchangia Matylda wakamsweka ndani yuko Segerea ananyea kwenye ndoo. Tanzania bwana mambo ya ukandamizaji siku hizi wazi wazi. Mnataka kuniambia Barabara na Elimu na Afya za Watanzania kipi bora. Hii miradi wanaojisifu nayoni kodi za Watanzania wamelipa na ukikaa kufanya mahesabu bado wameiba sana. Alimasi, Dhahabu, Tanzanite, Gasi, Makaa ya Mawe, Wanyama, Milima kweli tunadanganyiwa visima vya maji.
Mimi nashukuru Serekali imejenga barabara lakini kwa ujinga wangu nilionao sidhani hizi barabara zina faida yoyote kwa Watanzania kama fedha hizo zingetumika kufufua viwanda, Mashirika ya Umma, Mashule safi, Hosipitali safi, nk. Barabara mimi ningeshauri zisipewe kipaumbele kuliko Afya za watu na Elimu. Watanzania wangapi wanaouwezo wa kusafiri kwa kutumia hizo barabara. Watanzania wangapi wanazo hata baiskeli za kutumia hizo kilometa za barabara. Nchi imejaa Migomo kila mahali, Walimu, Madaktari, Magereza, nk.
 
 Watu wanadai Mishahara na marupurupu yao. Fedha nyingi sana za Watanzania zinatumika vibaya hasa kwenye kura. CCM inatumia mda mwingi sana kwenye kuchaguana. Angali ni mavazi aina ngapi wanavaa kwenye mikutano yao na chaguzi zao. Angalia fedha zinazotumika kwenye vipeperushi vyao. Watanzania lazima tubadilike. Watanzania tumetelekezwa na Serekali kwa kununua kila huduma. Kuanzia Elimu, na Afya. Bidhaa madukani hazishikiki mnasema maisha bora. Ukilinganisha rasilimali tulizo nazo na huduma zitolewazo na Serekali ya CCM ni udanganyifu mtupu. Lazima mabadiliko!
 
Mkereketwa
Lengai Ole Letipipi

No comments:

Post a Comment