MSANII mkali
wa Jumba la Sanaa Tanzania (THT) Ally Nipishe amesema baada ya ngoma yake ya
Mai kuendelea kufanya vizuri, anajiandaa kuja na ngoma nyingine mpya kabla
mwezi huu haujaisha.
Akizungumza
na safu hii, Ally Nipishe amesema anashukuru Mungu kwamba wimbo wa Mai umekubalika, ambapo amekuwa
akipata shoo mbalimbali ndani ya Dar es Salaam na bado watu wa mikoani wamekuwa
wakimtafuta kwa ajili ya shoo.
“Nashukuru
Mungu kwamba toka nimetoa wimbo wangu wa Mai unaendelea kufanya vizuri,
umekubalika kwa haraka kwasababu nimetoa ujumbe ambao ni wa kuelimisha jamii,
napata shoo pia,”alisema.
Ally Nipishe
amesema baada ya kuachia wimbo mwingine ambao hakupenda kuutambulisha kwa
haraka, anatarajia kufanya kazi na wasanii nyota akiwemo Ally Kiba na Young
Killer kwa vile ndio wasanii wanaomvutia kwa sasa.
Msanii huyo kipaji chake kilianza kuvuma pale
aliposhirikishwa na msanii wa kike anayetamba na ngoma yake kali ya Ni wewe,
Mwasiti Almas, ambapo alionekana kufanya vizuri na ndipo mashabiki kumtaka kuja
na wimbo wake ambao ndio unaovuma kona mbalimbali za redio nchini unaojulikana
kama Mai.
No comments:
Post a Comment