TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Monday 6 May 2013

TGNP kuzindua Ilani ya madai ya wanawake kwenye katiba mpya



Ussu Mallya
MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP) unatarajia kuzindua ilani ya madai ya wanawake kwenye Katiba mpya Mei 8, mwaka huu katika viwanja vya  Ofisi zake zilizopo Mabibo, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Ussu Mallya alisema TGNP kwa kushirikiana na wanaharakati wa masuala ya ukombozi wa wanawake, usawa wa kijinsia, haki za Binadamu, utawala bora na Maendeleo wamekuwa na utaratibu wa kuandaa ilani mbalimbali za wananchi kuanzia uchaguzi wa mwaka 2000, 2005 na 2010.

“Mwaka huu tumeandaa Ilani ya madai ya wanawake wa Tanzania kwenye katiba mpya, ili kuwezesha jamii kuchambua, kujadili na kuangalia maeneo muhimu ya kudai uwajibikaji na utekelezaji wakati wa mijadala ya kuandaa katiba mpya.

Alisema mchakato wa kuandaa madai ya katiba mpya umetokana na ushiriki mkubwa wa wadau mbalimbali yakiwemo mashirika katika ngazi ya kitaifa na jamii yanayotetea haki za Binadamu, jinsia na maendeleo, Femact na GDSS ambazo hufanyika kila Jumatano mabibo.

Kwa mujibu wa Mallya alisema madai hayo yametokana na ushiriki na sauti mbalimbali za wadau wanaotetea haki za wanawake na hususani haki zao za kikatiba na kuongeza kuwa ni matumaini yao kuwa tume ya mabadiliko ya katiba inatambua changamoto zinazowakabili wanawake ili yaweze kuingizwa katika katiba mpya.

No comments:

Post a Comment