TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Thursday 19 September 2013

TIC yaeleza mpango wa kuwaunganisha wajasiriamali

Meneja Mawasiliano wa Kituo cha Uwekezaji Bi. Pendo Gondwe (kulia) akieleza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mafuzo ya kitaalam waliyoyatoa  kwa wajasiriamali 285 katika Mikoa ya Dar es Salaam,Kilimanjaro, Mwanza na Mbeya ili kuwawezesha kukabiliana na ushindani wa kiuwekezaji na kufikia viwango vya kimataifa, wakati wa mkutano uliofanyika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Jijini Dar es Salaam leo.Kushoto ni Afisa Mwandamizi Huduma kwa Wawekezaji Kituo hicho Bw. Patrick Chove.

Afisa Mwandamizi Huduma kwa Wawekezaji wa Kituo cha Uwekezaji Bw. Patrick Chove akielezea kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) umuhimu wa wananchi kushirikiana na wawekezaji katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini, wakati wa mkutano uliofanyika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Jijini Dar es Salaam leo.Kushoto ni Kaimu Meneja wa Tafiti na Mipango wa Kituo hicho Bw. Njoki Tibenda.

PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO

No comments:

Post a Comment