TIMU ya Tanzania ya kuogelea ‘Swim
Squad’ imefanikiwa kutwaa medali 72 ilizoshinda kwenye mashindano ya
kuogelea ya Afrika Mashariki yaliyofanyika katika bwawa la Oshwal academy
Mombasa Kenya mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Msaidizi wa
Chama cha Kuogelea Tanzania(TSA) Ramadhan Namkoveka, katika mashindano hayo
yaliyoshirikisha nchi tatu za Uganda,
Tanzania na Kenya, Tanzania iliwakilishwa na wachezaji 42 na tayari ilirudi juzi
usiku na ushindi huo wa kuridhisha.
Alisema kati ya medali hizo, 22 ni medali za dhahabu 25 za fedha
na 25 za shaba. Kutokana na mashindano
hayo timu hiyo ya Tanzania imeshika nafasi ya tatu baada ya kujikusanyia alama
282 kati ya timu 27 zilizoshiriki.
Mshindi wa kwanza kwa wanawake ni timu
ya Braeburn ya Kenya iliyopata alama 466, ikifuatiwa na Seahorses ya Kenya
pia iliyopata alama 282.
Namkoveka alisema kwa wanaume timu ya
Tanzania Swim Squad imeshika nafasi ya pili na kukabidhiwa kikombe baada
ya kupata alama 271 ambapo mshindi wa kwanza ni Braeburn iliyopata alama 410 na
timu ya bandari ya Mombasa imepata alama 212.
Mchezaji bora kwa upande wa wanawake
miaka 12-13 ni Kimberly Hind wa Braeburn alama 24, Imara Thorpe kutoka Shule ya
Banda School mwenye alama 23 na Sonia Tumiotto wa Tanzania Swim Squad
kashika nafasi ya 3 kwa kupata alama 17.
Washindi wote hawa wamepata vikombe.
Mchezaji bora wanawake miaka 10-11
ambao pia wamepata vikombe ni Hadasa Mumbi Gichovi wa Loreto , Kenya ,
alitepata alama 37. W apili ni Gloria Muzito wa Dolphins ya Uganda aliyepata
alama 27 na wa tatu ni Emma Imholf wa Tanzania Swim Squad aliyepata alama 17.
Mtanzania Catherine Mason mwenye umri
wa miaka 16 anayesoma Mombasa wa timu ya Bandari ya Mombasa amekuwa mshindi wa
kwanza kwa wanawake kwa kupata alama 28, akifuatiwa na Natasha Owino wa
Seahorses ya Kenya aliyepata alama 25, na Akinyi Ogot wa Baracuda aquatic ya
Kenya amepata alama 20.
Kwa upande wa wanaume mchezaji bora ni
Tory Pragasa kutoka Bandari ya Mombasa amepata alama 45, wa pili ni Hilal Hilal
kutoka Tanzania kwa kupata alama 34 na Edward Ilako wa Seahorses ya Kenya
alikuwa wa tatu kwa kupata alama 17.
No comments:
Post a Comment