Miss Universe
Tanzania, Betty Boniface Omara ametamba katika maonyesho ya mavazi kwa warembo
85 wanaowania taji la Miss Universe la mwaka huu mjini Moscow.
Katika mashindano hayo
yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Vegas Mall, vazi la Betty lililobuniwa na
mbunifu anayekuja kwa kasi nchini, Mwanakombo Salim, lilipendwa na mashabiki
wengi na anamatarajio makubwa kushinda taji hilo wakati wa fainali za mwaka huu
zilizopangwa kufanyika Jumamosi.
Vazi hilo limechorwa
na wasanii wa Tingatinga, Said Kambili na Mimus, michoro ambayo ni maarufu
nchini iliyoasisiwa na msanii maarufu wa zamani, hayati Edward Tingatinga. Vazi
hilo hilo mbali ya kudumisha utamaduni wa Tanzania, pia limechorwa michoro
mbali mbali ya kuvitangaza vivutio vya kitalii.
Vazi hilo pia lina nakshi
za mkeka na miba ya mnyama maarufu
ajulikanaye kwa jina la Nungunungu. Vilevile pia umetumika kama njia ya
kumuonyesha ndege Tausi kama inavyoonekana rangi za mkeka kwenye mkia na
kilemba kichwani mwake.
Lengo kuu la nguo na
michoro hii ni kutangaza kazi za mikono na utalii wa Tanzania na miongoni mwa michoro
iliyoonyeshwa ni Duma, Tembo na Twiga vilevile imeonyesha ndege na mali asili
zipatikanazo Tanzania kama vile Tausi, vipepeo, mimea na Mlima Kilimanjaro.
Mashindano
ya Miss Universe Tanzania 2013 yamedhaminiwa na hifadhi ya Taifa Tanapa.
No comments:
Post a Comment