TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Saturday 23 November 2013

Wageni 'stop' biashara ndogo Zimbabwe

Rais Robert Mugabe wa Zimbambwe
Na Bbc Swahili
Wamiliki wa makampuni ya nje yanayoendesha shughuli katika baadhi ya sekta nchini Zimbabwe kuanzia Januari mosi mwaka 2014 hawataruhusiwa na iwapo watakiuka agizo hilo watakamatwa mmoja wa maafisa waandamizi wa serikali ya nchi hiyo amesema.

Katibu wa Uwezeshaji Uchumi George Magosvongwe alitoa onyo katika bunge la nchi hiyo, gazeti moja la serikali limesema.

Kumilikisha uchumi kwa wanyonge ni moja ya kampeni ya Rais Robert Mugabe katika uchaguzi uliofanyika mwezi Machi.

Kilimo, maduka ya kunyoa nywele, biashara za saluni, biashara ya kuuza vitafunio ni miongoni mwa kazi zitakazofanywa na wazawa pekee nchini humo.

"Kuanzia Januari mosi mwezi mmoja unaokuja tutaanza kuchukua hatua na tayari tumeandaa utaratibu na hatua za kuchukuka kwa wal watakaokiuka agizo hilo," Gazeti la serikali ya Herald limemnukuu Bwana Magosvongwe akisema.

Amesema raia wa Zimbabwe wamekwishaandaliwa ili kuchukua nafasi za kuendesha shughuli zilizokuwa zikiendeshwa na wageni ili kuepuka upungufu wa bidhaa.

Kwa mujibu wa gazeti la Herald biashara zilitengwa kwa wazawa ni pamoja na biashara za reja reja na jumla, maduka ya kunyoa, biashara za saluni, biashara za kutengeneza na kuuza vitafunio, kilimo , usafirishaji, biashara za majengo na matangazo.

Amesema migahawa inayomilikiwa na wageni ambayo haitengenezi vyakula vya asili haitaathirika.

Wamiliki wa biashara ambao hawatakidhi vigezo vya biashara za wazawa watakuwa katika hatari ya kupigwa faini au kifungo kama wataendelea kufanya biashara hizo gazeti la Herald limesema.

No comments:

Post a Comment