TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Tuesday 10 December 2013

Maelfu wamuaga shujaa wa Afrika Mandela

 
Na Bbc Swahili
Zaidi ya maraisa tisini wameungana na wananchi wa Afrika Kusini katika misa ya wafu ya Nelson Mandela na kusimulia kumbukumbu zao kwa Shujaa huyo wa Afrika.

Akiongea kwenye mkusanyiko huo mjini Soweto, Rais wa Marekani Barack Obama alimtaja Mandela kuwa shujaa na mkombozi wa Afrika na shujaa shupavu kuwahi kuonekana katika karne ya ishirini.

Alisema maisha ya Mandela lazima yawe mfano mzuri kwa dunia nzima hasa vita alivyopigania kuhakikisha utu wa watu unaheshimiwa.

Jamaa za Mandela wamemtaja baba yao Mandela kama mtu aliyetaka watu kuwa sawa.

Mmoja wa wajukuu wa Mandela alikariri shahiri la kusisitiza mshikimano wa watu. Obama alishangiliwa ingawa Rais Jacob Zuma anayehutubia wananchi alizomewa mara kwa mara.

No comments:

Post a Comment