Pongezi hizo alizitoa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na kusema "...Nimeambiwa kuwa asasi hii imesajiliwa kwa lengo la kuwashirikisha na kuwaunganisha vijana wenye vipaji vya sanaa na muziki pamoja na waliokwishafanikiwa katika kuwezesha kukuza vipaji walivyonavyo," alisema Bi. Kihimbi akimuwakilisha Katibu Mkuu.
"Kimsingi hili ni jambo jema la kusaidiana na
serikali katika kukuza vipaji na kuongeza viwango vya sanaa, ili
kuwawezesha wasanii wetu kukabiliana kikamilifu katika ushindani wa soko
la kimataifa," alisema.
"...Nawashauri vijana watumie fursa kama hii kila
kila zinapopatikana katika kufanikisha malengo yao kupitia fani za
sanaa. Kama sote tunavyofahamu kuwa sanaa ni ajira na inanafasi kubwa ya
kubadili maisha ya watu na nchi kiuchumi na kifikra ni vema watu
wakaondokana na dhana potofu kuwa sanaa si kazi ya maana na ni kwa
wasiohitaji kujifunza," alisisitiza.
Aidha alitoa changamoto kwa baadhi ya watu kuacha
fikra finyu za kuichukulia sanaa kama si kazi kama ilivyo kazi nyingine,
kwani mawazo hayo hayaitendei haki pamoja na kuzingatia umuhimi wa
sanaa kwa jamii.
"...Ninapata furaha kubwa kusikia kuwa tamasha hili
litakuwa likifanyika kila mwaka. Ninakupongezeni sana kwa kubeba sura ya
uzalendo unaolenga kuikuza, kuiendeleza na kuipa hadhi fani ya sanaa na
muziki," aliongeza.
"...Ninatambua kuwa kazi hii kubwa na nzuri
mnayoifanya ni utakelezaji wa sera ya utamaduni inayosisitiza na
kusimamia maadili ya Mtanzania pamoja na kuzingatia mafunzo na elimu
katika fani zetu. Tunafahamu kuwa utamaduni ni mali ya jamii, hivyo ni
jukumu la wananchi wenyewe kuupenda, kuuthamini na kuuendeleza utamaduni
wetu kwa kutumia kazi za sanaa."
Awali akizungumza kabla ya uzinduzi wa tamasha hilo,
Mkurugenzi Mtendaji wa UCA-Tz, Emmanuel Mushy aliishukuru Serikali kwa
ushirikiano iliouonesha kufanikisha tamasha hilo na kutoa shukrani kwa
makampuni ya Zantel, Coca Cola- Tanzania, Maezeki, LBGY Media na mtandao
wa Thehabari.com kushiriki kuwasaidia vijana wasiosikika kusikika.
Zaidi ya wasanii 25 chipukizi walipata nafasi kwenye
tamasha hilo ya kuonesha uwezo wao kwa jamii wakiwemo baadhi ya wasanii
chipukizi wanaoanza kunufaika na kazi zao kama Menina, M Rap na Ally
Nipishe.
No comments:
Post a Comment