Habari
zilizoufikia zinasema kuwa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu ya jijini Dar es Salaam imewaachia huru aliyekuwa
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima ambaye kwa sasa ni Mhariri
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, Absalom Kibanda, Meneja
Uendeshaji Biashara wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL),
Theophil Makunga, Mwenyekiti wa zamani wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson
Mwigamba.
Mahakama
hiyo imewaaachia huru watuhumiwa hao waliokuwa wakikabiliwa na kesi iliyodaiwa kuwa ilikuwa ni uchochezi baada ya kutoa hukumu leo katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi na watuhumiwa hao kuibuka kidedea kutokana na
ushahidi wa upande wa mashitaka kutojitokeza mahakamani hapo.
No comments:
Post a Comment