TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Wednesday 29 January 2014

Mahakama ya Kisutu yawaachia huru wanahabari Kibanda, Makunga na Makada wa Chadema washinda kesi dhidi ya uchochezi

Habari zilizoufikia  zinasema kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya jijini Dar es Salaam  imewaachia huru aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima ambaye kwa sasa ni Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, Absalom Kibanda,  Meneja Uendeshaji Biashara wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), Theophil Makunga, Mwenyekiti wa zamani wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
 
Mahakama hiyo imewaaachia huru watuhumiwa hao waliokuwa wakikabiliwa na kesi iliyodaiwa kuwa ilikuwa ni uchochezi baada ya kutoa hukumu leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi na watuhumiwa hao kuibuka kidedea kutokana na ushahidi wa upande wa mashitaka kutojitokeza mahakamani hapo.

No comments:

Post a Comment