TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Thursday, 22 March 2012

Nani atakuwa mkali kati ya Asha Ngedere na Salma?

Mchezaji wa ngumi wa kike Salma Kihombwa wa Morogoro akilonga jambo katika mahojiano katika ukumbi wa Habari Maelezo.                                                         





                                                                                                



                 



Asha Ngedere akiwa katika pozi akimaanisha amejiandaa kumkabili mpinzani wake Salma. ili kujua nani zaidi ni siku hiyo ya April 28, mwaka huu katika ukumbi wa PTA Sabasaba.







                                                                                                               

Asha Abobakari Nzowa 'Asha Ngedere' atamba kumpiga kipigo na mbwa mwizi mpinzani wake kutoka Morogoro Salma Kihobwa katika pambano la ndondi April 28, mwaka huu.

Jina la Asha Ngedere sio jina geni kwani ni maarufu kutokana na Zecomed kumtaja sana katika vipindi vyao vya TBC.

Ni kijana mdogo mwenye umri wa miaka 24 lakini mambo yake ni makubwa. Ili kujua nani zaidi kati ya Asha Ngedere na Salma  siku hiyo inasubiriwa kwa hamu.

Kwa mujibu wa Asha anasema kwanini uandikie mate wakati wino upo hivyo anahamasisha akina dada kujitokeza na kuona nani zaidi.

Kwake Salma mwenye umri wa miaka 17 anasema Asha bado mtoto atampiga hadi atambae kwa miguu. Hayo yote ni maneno tu kinachosubiriwa ni siku hiyo.
Shindano hilo limedhaminiwa na Kitwe General Traders.

No comments:

Post a Comment