TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Thursday, 22 March 2012

Cheka na Maugo watambiana kuchukua ubingwa


Fransis Cheka 'SMG' kushoto akiwa na Mada Maugo wakionyesha mkanda wa IBF Afrika utakaogombaniwa rasmi katika pambano litakalofanyika April 28, mwaka huu katika ukumbi wa PTA Sabasaba. Mshindi anatarajiwa kuondoka na gari.     














                                                                
           












Bondia wa ngumi za kulipwa nchini Francis Cheka ‘SMG’, wa Mji Kasoro Bahari Morogoro, ametamba kutoa kipigo kikali  kwa mpinzani wake Mada Maugo ‘Mbunge wa Rorya’ wa jijini Dar es Salaam.

Cheka na Mada  wanatarajiwa kuwania ubingwa wa IBF, uzito wa Middle raundi 12, pambano litakalofanyika ukumbi wa PTA Sabasaba jijini Dar es Salaam, ambapo limepangwa kufanyika Aprili 28 na kusimamiwa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC).

Cheka anasema kichapo kiko pale pale kwani amejiandaa vizuri na kwasababu yeye ni bingwa hamwogopi Mada kwa vile aliwahi kumpiga mara 2 , na kumpiga Rashid Matumla mara 4 hivyo haoni sababu ya kushindwa.

“Nitamchapa Maugo katika raundi za awali tu, kwani najiandaa vilivyo ili nisiharibu rekodi yangu kwa mwaka huu,” alisema Cheka.

Kwa upande wake Mada Maugo alisema kwa sasa amejipanga na anaamini kuwa mkanda utakuwa ni wake, hatokubali uende kwa Fransis Cheka.

Pia, kutakuwepo na pambano la wanawake ambapo Asha Ngedere ametamba kumpiga kipigo cha mbwa mwizi Salma Kihombwa wa Morogoro. Kila mmoja anatamba kummaliza mwenzake.

Akizungumzia kuhusu  pambano hilo Promota wa pambano hilo Lucas Rutainurwa alisema tayari mkanda umeshawasili kutoka Marekani kinachosubiriwa kwa sasa ni pambano kwani kila kitu kimekamilika.

Mdhamini  wa gari katika pambano hilo ambaye ni Moses Katabaro wa kampuni ya Kitwe General Traders alisema gari ameshakabidhi lengo ni kuhakikisha kuwa mchezo wa ngumi unachukuliwa kama ajira.

“Natoa kipaumbele katika mchezo wa ngumi lengo ni kutambulisha mchezo huo ili hatimaye wachezaji wauchukulie kama ajira muhimu kwao, gari tumekabidhi tunachosubiri ni ushindi siku hiyo,”alisema.

No comments:

Post a Comment