TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Thursday 5 April 2012

Jamii ya Tanzania iondoe woga kupigania ardhi yao


Wengi wanaonenaka kutokuwa na elimu ya kutosha ndio maana wanaendelewa kukandamizwa na mfumo unaoendeshwa na Serikali.

Mada iliyokuwa ikiendeshwa katika semina za GDSS ambazo hufanyika kila Jumatano katika viwanja vya Mtandao wa Jinsia Tanzania ilikuwa ikisema ‘Historia ya Uporaji Ardhi katika Muktadha wa katiba Tanzania’

Mtoa mada katika semina hiyo alikuwa ni Dk. Ngwauza Kamata kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo alisema mfumo uliopo umelenga kuwakandamiza watanzania bila kujua kwani wengi hawana uelewa na kile kinachoendeshwa na serikali.

Serikali ya Tanzania imekuwa ikitangaza ardhi ya Tanzania kwa wageni na kuwaacha watanzania wengi wakiwa ni watu wa kutanga tanga kwani kila kukicha utasikia mgogoro wa ardhi ya mwekezaji na wananchi.

Kwa mujibu wa Dk. Kamata ni kwamba kwa sasa watu wengi kwa sasa wanalala nje kuliko miaka ya 80. Kumekuwa na ongezeko la majengo marefu lakini mengi hujengwa kwa ajili ya kukodisha ofisi na sio kwa ajili ya wananchi kukaa.

Lakini ili wananchi waweze kufanya mapinduzi makubwa kutetea ardhi yao ili isiendelee kuuzwa kiholela kwanza jambo la muhimu linasisitizwa na Dk. Kamata wananchi kujiandaa na kujipanga kwa maana ya kuwa na umoja ili kudai haki zao.

Na kujipanga huko sio tu kuzungumza kwa maneno bali kwa vitendo kama ambavyo nchi nyingine zimekuwa zikifanya na kufanikiwa. Botswana ni moja ya nchi ambayo ilifanikiwa kutetea ardhi yake.

Baadhi ya wana GDSS wengine walisema kwanza umiliki wa ardhi kwa wananchi uingizwe kwenye katiba mpya. Serikali isiendelee kuwapora wananchi ardhi yao na kuwaacha wakitangatanga ndani ya nchi yao.

Lakini zaidi wanasisitiza wanawake wapewe nafasi ya kumiliki ardhi.  

No comments:

Post a Comment