TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Monday 2 April 2012

Mabalozi wa Umoja wa Ulaya, Norway wazuru mkoa wa Mtwara



Mabalozi tisa wa Umoja wa Ulaya pamoja na mwenzao kutoka Norway walitembelea mkoa wa Mtwara ambapo walifanya mazungumzo na wadau wa maendeleo kuhusu mambo mbali mbali yahusuyo mkoa huo pamoja na shughuli na matarajio ya baadae katika sekta ya gesi asilia.

Ziara hiyo iliongozwa na Balozi Filiberto Ceriani Sebregondi, ambaye ni mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Ulaya kwa Tanzania, ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa kundi hilo. Ilijumuisha wanadiplomasia kutoka katika balozi zilizopo Tanzania za nchi za Ubelgiji, Denmark, Finland, Ufaransa, Ujerumani, Hispania, Sweden na Uingereza. Balozi wa Norway pia alishiriki pia katika ziara hiyo. 

Wakuu hao wa balozi za nchi zao hapa Tanzania walitembelea Bandari ya Mtwara, Kisima cha kuchunguza uwepo wa mafuta baharini, mtambo wa kutengeneza gesi na mtambo wa kuzalisha nishati kwa kutumia gesi uliopo jirani na bandari hiyo. Pia walifanya mikutano na maofisa wa serikali mkoani humo akiwemo Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Bi. Hasna Mwilima, na wadau wengine.

Akizungumza punde baada ya ziara hiyo, Balozi Sebregondi aliainisha umuhimu wa ugunduzi mpya wa rasilimali asilia nchini Tanzania kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kuitaka serikali kuchukua hatua za kukabiliana na changamoto ambazo zinaweza kujitokeza kutokana na ugunduzi huo.

"Dalili njema katika sekta ya gesi ya Tanzania zinatoa fursa ya kipekee kwa ajili ya kuharakisha maendeleo ambayo yanaweza kuleta faida kubwa kwa watu wa Tanzania," alisema huku akidokeza kuwa uzoefu kutoka maeneo mengine duniani umeonesha kuwa hili huwa linakuja na changamoto nyingi ambazi zinahitaji kufanyiwa kazi.

"Hii inatoa fursa kwa Umoja wa Ulaya na wabia wengine kufanya kazi kwa njia zenye ubunifu na serikali pamoja na sekta husika kupunguza hatari zinahusiana na maendeleo haya ili kuiwezesha Tanzania kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini," alisema.

No comments:

Post a Comment