TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Monday 2 April 2012

Kabula alonga ujio wa albam yake mpya ya nitang’ara tu




Baada ya kimya cha takribani miaka miwili sasa hatimaye Mwimbaji wa muziki wa Injili nchini Kabula George ameamua kurudi tena katika sanaa ya muziki wa injili kwa kishindo kwa kutoa albam yake mpya  inayobebwa na wimbo wa nitang’ara ikiwa imebeba ujumbe wa kumsifu Mungu.
Mwimbaji huyo anayefahamika ndani na nje ya nchi kutokana na uimbaji wake ameliambia gazeti hili kuwa wimbo wa nitang’ara ukiwa  pamoja na nyimbo nyingine sita zimeanza kusikika katika redio mbalimbali, ila kwa upande wa video wameanza mchakato wa kurekodi ambapo hadi mwishoni mwa mwezi huu itakuwa imekamilika.
Nyimbo sita zilizoko katika albam hiyo ni Nitang’ara, Majaribu, Nimesogea, Nataka kumwona Yesu, Ni mwema  na peleleza ambazo zote zimelenga kutoa elimu kwa jamii hasa wale wanaomwamini Mungu na hata wasioamwamini Mungu wakisilikiza watabarikiwa.
Anasema “Namshukuru Mungu kwasababu nimefanikiwa kurekodi nyimbo zangu sita katika audio na sasa tuko katika kurekodi video na nawaeleza mashabiki wa muziki wa injili kwamba mwishoni mwa mwezi huu itakuwa sokoni hivyo naomba watuunge mkono katika kumsifu Mungu,”.

Kabula anaelezea jinsi ambavyo aliguswa kutunga wimbo wa  nitang’ara  ambao ndio uliobeba albam yake kwamba  wimbo huu aliupata baada ya kupitiaa katika maisha magumu yaliyosababisha baadhi ya majirani zake kumbeza kutokana na changamoto alizokuwa  akizipitia .

“Nimepita katika nyumba mbalimbali ambazo majirani walikuwa hawaishi kunibeza. Nikiwa katika hali ya kuutafakari uweza wa Mungu kwa kuona kama ameniacha ndipo nilipopata wimbo huu,”anasema Kabula.

Wimbo huo aliupata kutokana na kuongeza juhudi za maombi kwa kuamini kuwa siku moja atang’ara licha ya kupita katika changamoto hizo ambazo wamekuwa wakizipata watu mbalimbali hasa wanaoishi kwenye nyumba za kupanga.

Anasema kuwa kupitia wimbo huo, tayari kuna baadhi ya watu umewagusa kwa namna moja ama nyingine kwani amekuwa  akipata simu mbalimbali za kumpongeza hasa ukizingatia kuwa ni  wimbo unaozungumzia maisha hivyo umewagusa wengi wanaokutana na changamoto za namna hiyo,  wanaamini siku moja watang’ara.

Historia
Kabula George alianza kuimba  muziki  wa injili akiwa bado ni mtoto mdogo, mazingira aliyolelewa ya kumsifu Mungu yalimfanya  kuwa na moyo wa kuendelea kuhudumia watu kupitia uimbaji.

Mwaka 2003 alijiunga na kwaya ya Uinjilisti ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Kinyerezi, ambapo aliimba kwaya hadi mwaka 2005 alipoolewa na Mume wake George Kayala ndipo alipoamua kurekodi ili  kuendeleza huduma hiyo.

Albam yake ya kwanza aliitoa mwaka 2005 ilibebwa na wimbo wa Amani lakini kutokana na matatizo ya hapa na pale akaelezwa kuwa haina ubora unaohitajika hivyo mwaka 2007  akurudia kurekodi tena huku akichukua baadhi ya nyimbo na kuzirudia akabadilisha jina na kuiita  ‘PESA’

Alibamu hiyo iliingia sokoni na ilifanya vizuri  wakati huo. Mwaka 2009 alifanikiwa kurekodi albamu ya pili iliyojulikana kwa jina la Ushindi. Ambapo ndani yake  kulikuwa na wimbo wa dhihirisha ambao ulionekana kupendwa sana na watu na kumtambulisha katika anga ya muziki wa injili.

No comments:

Post a Comment