TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Wednesday, 4 April 2012

Makala awaeleza wadau wa utetezi wa haki za walemavu kuendelea kutoa huduma kwa walemavu


KAMISHNA wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dunford Makala amewataka wadau wa utetezi wa watu wenye ulemavu kuendelea kushirikiana katika kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu nchini.

Akizungumza katika mkutano wa ufunguzi wa wadau wa utetezi wa masuala ya watu wenye ulemavu Kamishna Dunford Makala alisema Wizara kupitia idara ya ustawi wa jamii imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya utoaji huduma kwa watu wenye ulemavu na waishio katika makazi ya wasiojiweza, sambamba na kuendeleza vyuo vya mafunzo ya ufundi stadi kwa watu wenye ulemavu.

“Ushirikiano wetu wa hali na mali ndio utasaidia kuboresha maisha na huduma kwa watu wenye ulemavu na wizara kupitia idara ya ustawi wa jamii imeendeleza ushiriki wake kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya huduma kwatu wenye ulemavu pamoja na kuendeleza vyuo vya ufundi stadi” alisema.

Aidha aliongeza kuwa pamoja na hayo changamoto inayowakabili ni ufinyu wa bajeti inayotolewa na serikali kwa ajili ya huduma hizo, pia alisema kanuni za sheria ya watu wenye ulemavu imesahapita katika hatua zote za awali na sasa iko kwa Mwanasheria Mkuu kwa ajili ya mapitio.

Mwenyekiti wa SHIVYAWATA Lupi Maswanya aliwashukuru wadau kwa kuendelea kutoa ushirikiano wao wa hali na mali kwa kukubali na kutambua ushirikianon wao.

No comments:

Post a Comment