Afande Sele akitumbuiza katika moja ya matamasha yake |
Hadi sasa
tayari ameshatoa burudani katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Akizungumza
na gazeti hili jana alisema ndani ya wiki hii anatarajia kwenda kuburudisha
katika mikoa ya Mbeya, Songea, Iringa na mikoa mingine ambapo atadhaminiwa na
Kinywaji cha Pepsi.
Alisema
Kinywaji hicho kimemdhamini kupiga shoo mikoani ambapo pamoja na burudani pia
April mwaka huu aliteuliwa kuwa Balozi wa Pepsi na kwamba amesaini mkataba wa
kufanya nao kazi hadi Desemba mwaka huu.
“Nashukuru
Mungu kinywaji cha Pepsi kimeniteua kuwa Balozi wake na kimenidhamini katika
shoo zangu ambapo nitaenda kupiga karibu mikoa yote ya Tanzania, nachosisitiza
ni mashabiki mbalimbali kujitokeza pindi tutakapofika mikoani ili kutuunga
mkono,” alisema.
Mbali na
hilo, Afande Sele kwa mwaka huu tayari ameshatoa wimbo uitwao ‘Mr. President’
ambao umekuwa ukichezwa katika baadhi ya vyombo vya habari. Kinachomsikitisha
ni kuona kuwa nyimbo zenye ujumbe zinawekwa pembeni huku zile za mapenzi
zikipigwa sana.
Alisema nyimbo
zao zimekuwa hazichezwi sana kwenye redio kutokana na chuki binafsi za baadhi
ya watu, lakini anachoshukuru ni kuona kuwa kuna watu wanafuatilia kwenye
mtandao na kuzisikiliza hivyo anapata moyo wa kuendelea kuimba.
Afande
alisema baadhi ya watu wamekuwa wakimuhoji kwamba yuko kimya hasikiki wakati
kila mwaka hutoa nyimbo mpya ila tatizo ni baadhi ya watu kutozipiga nyimbo
zake jambo ambalo hata mashabiki wake wamekuwa wakiamini pengine ameacha muziki
wakati bado yuko sokoni.
No comments:
Post a Comment