Ally J wa kwanza kushoto akizungumza jambo |
RAIS wa
kundi la Five Stars Modern Taarab, Ally Juma ‘Ally Jay’ amesema, anasikitika
kuona kuwa kuna watu wanaoamini kwamba, amehusika kuwatoa kafara wasanii
wenzie, kwenye ajali iliyolikumba kundi lao, Machi 21, mwaka jana.
Ally J,
mahiri kwa upapasaji kinanda, aliyasema hayo kwenye mahojiano na kipindi cha
Shamsham za Pwani, kinachorushwa kila wiki, katika siku za Jumamosi, kwenye
runinga ya ITV.
“Unajua,
kuna wengine hawaamini kuwa nami nilikuwamo kwenye gari iliyopata ajali siku
ile, eti kwa sababu tu nilinusurika na kutoka bila jeraha,” alisikitika Ally
Jay.
Alisema
kuwa, ajali ile ni mipango ya Mwenyezi Mungu, ambako hata yeye aliguswa vilivyo
na kuzidi kuumia kila anapowakumbuka wasanii wenzie waliopoteza maisha kwenye
tukio hilo .
Aidha,
Ally Jay aliiomba jamii kuachana na fikra potofu za kuhusisha matukio ya maafa
na vifo vya wasanii na imani za kishirikina, ambako alisema kuwa hali hiyo
husababisha migongano mikubwa.
Alisema,
mara nyingi yanapozuka matukio ya namna hiyo, wanajamii huwa wepesi kukurupuka
kutafuta mchawi, huku wakisahau kuwa kila jambo linapangwa na Mungu.
No comments:
Post a Comment