Dk.Fenella Mukangara |
Waziri
wa Habari, Utamaduni na Michezo Dr. Fenela Mukangara anatarajiwa kufunga
mashindano ya fainali za mchezo wa bao Jumamosi hii ambapo timu nne kati ya
tisa zilizoshiriki mashindano hayo zilifanikiwa kutinga fainali katika michuano ya mchezo hiyo.
Katika
mashindano hayo ambayo yalianza rasmi April 26 mwaka huu ikiwa ni sehemu ya
kuadhimisha miaka 48 ya Muungano jumla ya timu tisa zilishiriki ikiwa ni pamoja
na Mlaponi, Mtea, Muungano, Nyayo na Kilamba, Uyaga, Kopa, FFU na Magereza.
Akizungumza
na blogu hii kwa njia ya simu Rais wa
Shirikisho la Mchezo wa Bao Tanzania (Shimbata) Monday Likwepa alitaja timu nne
zilizofanikiwa kutinga fainali kuwa ni pamoja na Mlaponi na Uyaga ambazo
zinaoongoza zikifuatiwa na Kopa na Muungano.
“Tumeshapa
timu nne zilizoingia fainali na tunategemea Jumamosi zitakapochuana ili kupata
mshindi Dk. Mukangara atakuwa ndiye mgeni wetu atakayetoa zawadi kwa washindi
wa mashindano hayo,”alisema Likwepa.
Alisema
mshindi wa kwanza anatarajiwa kunyakua kitita cha shilingi 400,000, wa pili
200,000 na wa tatu 100,000 wakati mshindi wan ne atanyakua 80,000. Pamoja na
hao, mfungaji bora atanyakua 40,000, nidhamu ya bao 40,000, kamisaa bora 30,000
na kifuta jasho ni shilingi 20,000 kwa kila mmoja.
No comments:
Post a Comment