Rais wa bendi
ya Mashujaa musica Chars Siprian ‘Chars Baba’ amesema anasubiri kumalizia
kibanda chake ndipo amtambulishe mchumba wake mpya na kufunga naye ndoa.
Msanii huyo wa
dansi ambaye aliwahi kutamba katika bendi ya Twanga Pepeta alisema kwa sasa hawezi
kumtambulisha hadi hapo atakapotimiza
malengo yake hasa kumalizia nyumba yake.
Chars kwa
sasa ni baba wa watoto wawili kwa mama tofauti huku mmoja akizaa na msanii
mwenzake Sajenti Husna. Hata hivyo, alisema wameshaachana na Husna na tayari ni
mchumba wa msanii wa dansi wa kundi la Mapacha.
Pamoja na
hayo, alitambulisha wimbo mpya ambao Bendi ya Mashujaa imeuachia hivi karibuni
unaojulikana kama Risasi kidole akimaanisha kuwa watu wengi wanapenda
kuwanyooshea kidole wale ambao wameishiwa na kuwasema vibaya jambo ambalo sio
zuri.
Hivyo wimbo
ni elimu tosha dhidi ya wale wote wanaopenda kusema sema watu vibaya.
No comments:
Post a Comment