BAADA
ya kutamba na wimbo wake wa ‘nasemwa semwa’ msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini wa THT,
Nash Dizaina ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Ujinga
huo ambao ameutengeneza mwenyewe .
Akizungumza
jijini Dar es Salaam, Nash alisema wimbo
huo tayari umeanza kusikika katika vituo mbalimbali vya redio na kwamba
mashabiki wake waufuatilie ili wapate kuburudika.
"Nimefanya
vizuri sana katika wimbo huo kutokana na ubunifu ambao nimeufanya hali
inayoashiria naweza kurudi tena kwenye chati ya muziki wa bongo fleva kwa muda
mrefu sasa," alisema Nash
Pia,
msanii huyo aliwaomba mashabiki wa muziki huo kumpa ushirikiano wa kutosha
katika wimbo huo kwa kumuunga mkono hasa pale atakapokuwa katika shoo ambazo
hupiga Maisha kila mwishoni mwa wiki.
Mbali
na wimbo huo aliwahi pia kuvuma na wimbo wa 'No time' ambao aliimba remix ikiwa
ni kopi kutoka kwa msanii wa Nigeria Brackets.
No comments:
Post a Comment