Msanii wa Bongo fleva nchini Naseeb Abdul ‘Diamond’
anatarajiwa kumsindikiza mzee wa Nai nai, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ wakati
anatambulisha wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Baadae’.
Akizungumza
na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana, Ommy alisema Baadae ni wimbo wake
mpya ambao atautambulisha kwa mashabiki wake Jumapili ndani ya ukumbi wa
Bilicanas uliopo Posta mpya jijini Dar es Salaam.
“Diamond
namkubali sana ndio maana nimemuomba anisindikize kuitambilisha kazi yangu mpya
ambayo najua mashabiki wangu wanaisubiri kwa hamu sana” alisema Ommy.
Alisema
kazi hiyo ipo kwa upande wa audio peke yake na kwasasa anajipanga kwenda nchini
Afrika Kusini kwaajili ya kufanya video ya wimbo huo.
Ommy
ambaye alikuwa ni miongoni mwa wasanii waliopata tuzo ya Kilimanjaro aliwaomba
mashabiki waweze kufika kwa wingi katika shoo yake, na kutaka wasubiri mambo
mazuri kutoka kwake kwani kuna mambo mengi aliyowaandalia.
No comments:
Post a Comment