NYOTA
wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ismail Seif ‘Suma Lee’ kaachia wimbo
wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Utamkumbuka’ ambao kamshirikisha
mtayarishaji wa muziki huo Khalifani Majani ‘P.Funk’.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Suma Lee alisema wimbo huo
katengeneza tofauti na nyimbo zake nyingine kwa lengo lakuwapa radha
tofauti mashabiki wake.
“Wimbo
naamini utafanya vizuri zaidi na mashabiki wangu wataupenda kupita
kiasi hivo nawaomba wapenzi wangu waeendelee kunipa sapoti katika kazi
zangu” alisema Suma Lee.
Alisema wimbo huo kautengeneza katika Studio ya Bongo rekodi na imetengenezwa na watayarishaji mahiri pamoja na P.Funk mwenyewe.
Mbali
na wimbo huo, Suma Lee alishawahi tamba na nyimbo zake kama Hakunaga,
Chungwa na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika
vituo mbalimbali vya redio na luninga.
No comments:
Post a Comment