Msanii wa Bongo Fleva Dito amesema ana mpango wa kufungua tovuti yake ambayo ataweka mambo yake yote huko na itakuwa rahisi kwa mashabiki wake ambao wanataka kufuatilia kwa
karibu yale ninayofanya kuyapata kiurahisi.
Dito anasema
tovuti atakayofungua ataweka muziki wake kwa maana na video na audio, historia
ya maisha yake, shughuli zake ambazo anazifanya na mambo yote yanayomuhusu.
Hivyo, itakuwa ni nafasi nzuri kwa mashabiki wake kutembelea tovuti yake mara
atakapoifungua siku za karibuni.
Anasema kuwa
“Nitakapoifungua ni wazi kwamba nitaitangaza kwa mashabiki wangu wasiwe na
wasiwasi, pia sio tu kwa watanzania watakaonufaika bali pia hata kwa marafiki
wengine nje ya nchi itawarahisishia kuzifahamu kazi zangu kiurahisi,”.
Dito anasema
anataka kubadilika kuendana na wakati hasa ikizingatia kwamba dunia ya leo
imebadilika, pia kuna mabadiliko ya sayansi na teknolojia. Kitendo cha yeye
kutaka kuja kivingine ni kwa vile anataka kubadilika kwa kadri dunia
inavyobadilika ili kuendana na wakati.
Pamoja na
hayo, Msanii huyo anajivunia mafanikio mbalimbali aliyopata kimuziki ingawa
anasema sio kwa sana lakini anachokipata kutokana na muziki kinamwezesha
kusonga mbele kimaisha.
Anasema sio
sawa na kukaa bure kwasababu muziki unamlipa kwa kiasi. Wasanii wengi hutoa
wimbo mmoja mmoja ili wapate shoo kwasababu wanaamini ndio inayolipa zaidi kuliko
albam.
Dito anasema
kama Rais angempa nafasi ya kuzungumza kero yake ambayo angeizungumza ni wizi
wa kazi za wasanii. Sio kwamba msanii huyu ni kwanza kuzungumzia tatizo hili bali
karibu wasanii wote wamekumbwa na tatizo hilo nab ado wanalia kubiwa.
Anasema kuna
haja kubwa ikatolewa elimu kwa wasanii na jamii kwa ujumla kuhusiana na tatizo
hili. Wasanii wengi hawanufaiki ipasavyo kwasababu ya kazi zao nyingi kuibwa.
Dito
anaamini elimu pekee inaweza ikaleta mabadiliko makubwa kwa jamii. Anasema
inahitaji kuelimishwa ili isiendelee na tatizo hilo la kuiba kazi zao.
Pamoja na
hayo, Msanii huyo kwa sasa ameachia kibao kingine kikali kinachoitwa ‘niamini’
ila bado hajakiachia mtaani kwani anaendelea kukitengeneza na siku ikifika
wakati wowote kitasikika.
Hivyo,
anawaeleza mashabiki wake kuwa mwaka huu wataona mambo mengi mapya ikiwa ni
pamoja na kuwaletea nyimbo kali kama ilivyo kawaida yake.
Mwaka 2007 Dito alivuma katika singo ya Ulibisha
Hodi na kutoka tena 2009 akiwa katika kundi la Lafamilia lililokuwa chini ya
Chid Benz katika wimbo wa Dar es Salaam Stand Up.
Dito tayari ana albam yake ya kwanza yenye nyimbo 10 ambazo ni pamoja na Wapo,
Kwa Pamoja, Si Ulisema, Mdomo ft Linah, Kidogo ft Mh Temba , Sikumwelewa, Kaluma
ft Koba, tushukuru na nyingine.
Kwa wale
wanaofuatilia muziki wa bongo fleva kwa muda mrefu watakumbuka kuwa mwanamuziki
huyo alianza kusikika kwa mara ya kwanza
aliposimama na mfalme wa Rhymes Afande Sele katika wimbo wa Darubini kali ikiwa
ni miaka ya 2004.
Wimbo huu
ulivuma na kumpa umaarufu enzi hizo alikuwa akifahamika kama Dogo Dito mpaka
pale alipokuja kutoa Dunia ina mambo mwaka 2005 akiwa na tena na Afande Sele.
Ni mwanamuziki ambaye sio tu ni mzuri katika kutunga mashairi bali pia
anajivunia kuwa na sauti nzuri inayowavutia wengi pale ambapo yuko stejini
akiimba.
|
No comments:
Post a Comment