TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Wednesday 16 May 2012

JATA yapata mdhamini wa mashindano wa Judo


Chama cha Judo Tanzania (JATA) kimempata  mdhamini wake mkuu  ambaye ni Yuliy Tarverdyan ambaye ni Meneja  wa Kampuni ya Gemini Corporation Ltd atakayedhamini mashindano  ya kitaifa ya mchezo huo yatayotarajiwa kutimua vumbi  Mei 26 na 27 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Chama hicho Khalifa Kiumbemoto  ‘Chief  Kiumbe’ alisema mfadhili huyo ni raia kutoka Urusi  na ni mfadhili wa kwanza kujitokeza katika Uongozi  huo mpya ambao unaongozwa na yeye.

Alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa mashindano hayo  yatakuwa ni ya kwanza kufanyika nchini ambapo zaidi ya wachezaji 100 kutoka Tanzania Bara na Visiwani wanatarajiwa kushiriki katika mashindano hayo yatakayofanyika katika Hotel ya Landmark.

“Tunashukuru sana Kampuni hii kwa kujitokeza ili kutuunga mkono, kwani  ni fursa hii ni ya kipee na haijawahi kutokea katika tasnia ya mchezo huu hapa nchini, tunaamini kwamba mashindano ya kuwalipa washindi pesa itasaidia kukuza viwango,”alisema.

Alitaja zawadi kwa washindi kuwa mshindi wa kwanza atapewa dola 600 kulingana na kilo, mshindi wa pili atapata dola 300, mshindi wa tatu dola 100 pamoja na medali na cheti cha ngazi ya Diploma.

Naye  Yuliy tarvedyan ambaye ndiye mdhamini wa mashindano hayo alisema anatarajia kutoa  fedha zaidi ya dola 25,000 ikiwa ni udhamini wake katika mashindano hayo.

Alisema kampuni yake ya Gemini imepanga kudhamini mashindano ya kitaifa na kimataifa ya mchezo huo ili kuinua mchezo huo ili hatimaye JATA iweze  kufikia malengo yao na kuwawezesha vijana wengi kuupenda mchezo huo.

“Tunaamini kwamba kutoa zawadi za fedha kwa wachezaji kutaleta matokeo mazuri ya mchezo huo na kuwafanya wachezaji kujitahidi kushindana kwani tunahitaji kupata wachezaji wazuri watakaoshindana kitaifa na kimataifa,”alisema.

Tarvedyan alisema vifaa mbalimbali kwa Club zote nchini kwa Tanzania bara na Visiwani kwa ajili ya kujiandaa na mchakato wa mashindano.

No comments:

Post a Comment