Akiongea na Waandishi wa Habari katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mahusiano wa Kampuni ya SBL Bi. Teddy Mapunda, alisema hadi sasa wameshapata washindi wawili wa jenereta ambapo tayari wamewakabidhi zawadi zao, wengine ni washindi wa bajaj moja na wa pikipiki moja ambao nao wameshakabidhiwa zawadi zao.
Hata hivyo, zaidi ya milioni 780 zinashindaniwa
katika promosheni hiyo. “Tunawashauri wateja wetu na watanzania wote wenye sifa
za kushiriki katika promosheni hii kwa wingi bila kukata tamaa na hatimaye nao
waweze kushinda kwani promosheni yetu ni ya kweli, ya uhakika na ya haraka.”Alisema.
Aliongeza
kuwa mpaka sasa tayari watu zaidi ya
2000 wamejishindia pesa taslimu na wakafanikiwa kupata pesa hizo kwa urahisi
kabisa kupitia mtandao wa kutuma na kupokea pesa wa kampuni ya mawasiliano ya
simu za mkononi Vodacom MPESA ndani ya masaa ishirini na nne. Pia, washindi wamepatikana
ambao wamejishindia zawadi za vinywaji vilivyopo katika promosheni hiyo.
Bw. Ibrahim ambaye hakuwa na kazi yoyote mpaka bahati iliyobebwa na promosheni hii ilipomdondokea alikuwa na haya ya kusema, “kwa kweli nilipopata taarifa ya kushinda zawadi ya pikipiki sikuamini lakini sasa nimeamini na nawashukuru sana SBL kwa kuwa sasa naweza kujiajiri na kuendeleza maisha yangu na wale wanaonitegemea”. Kutoka jijini Mwanza Godfrey Shao ambaye alijinyakulia bajaj ya gurudumu tatu anaendelea kusubiri taratibu za usajili zikamilike ili aweze kukabidhiwa bajaj yake.
Aidha, kampuni hiyo iliendesha droo ya tatu leo na kupata washindi wengine ambao ni pamoja na Fadhili Manzi mkazi wa Mafinga mywaji wa bia ya Serengeti Premium Lager ambaye amejishindia bajaj na Raymond Denis mkazi wa Iringa ambaye amejinyakulia jenereta kupitia bia ya Tusker Lager.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment