TGNP kufanya mafunzo ya uraghibishi mikoa mitatu
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP)
utafanya mafunzo ya uraghibishi ngazi ya jamii kwa mikoa mitatu ya Shinyanga, Morogoro na Mbeya,
ambapo katika mikoa hiyo watajikita
katika wilaya za Mbeya vijijini,
Morogoro Vijijini na Kishapu. Mafunzo
haya yataanza tarehe 22 – Mei 2011 – 2 June 2012.
Mafunzo hayo yana malengo ya kuwajengea
wananchi uwezo wa kushiriki, kuchambua kwa kina fursa na changamoto
zinazowakabili katika mazingira yao na kuyatafutia ufumbuzi kwa kujenga vuguvugu la ukombozi wa wanawake
kimapinduzi.
Matarajio ya matokeo makubwa ya Mafunzo ya Uraghibishi na utafiti shirikishi wa kijamii,yatawashirikisha
wanawake na wanaume walioko
pembezoni katika kutambua fursa
walizonazo katika kudai au kuingizwa kwa madai
yao katika mchakato wa Katiba mpya, kudai mabadiliko ya sera,
kimfumo, na haki ya uchumi kwa makundi
yaliyoko pembezoni.
Mafunzo haya pia yatawajengea
wanajamii uwezo wa kushiriki ipasavyo katika mchakato wa kutoa maoni kwa Tume
ya Kuratibu Mchakato wa katiba mpya, haki ya uchumi, na maisha endelevu kwa
wote.
Baada ya mafunzo haya, wanajamii
wataibua vipaumbele vya changamoto zinazowakumba na watajadili namna ya
kukabiliana nazo wakiwa na viongozi wa serikali ngazi ya wilaya,kata na vijiji.
Mwisho TGNP itaendesha warsha kwa wanajamii namna ya kuanzisha na kusimamia vituo vya taarifa na maarifa
katika wilaya zao ikiwa ni sehemu ya kukutana na kushirikishana uzoefu na
kujadili masuala mbali mbali
zinazowakabili.
Imetolewa na
Usu
Mallya
Mkurugenzi
Mtendaji wa TGNP
No comments:
Post a Comment