Wafanyakazi
wa viwanda vya kubangua korosho vya Lindi, Mtwara, Pugu na Kibaha wamevamia
Ofisi za Bodi ya korosho kwa mabango na nyimbo za kudai haki zao wakitaka Bodi
hiyo iwalipe mafao yao wanayodai kwa muda mrefu.
Wafanyakazi hao
walikuwa wakiimba “tunataka haki zetu, tunataka haki zetu huku wengine
wakizungumza kwa hasira dhidi ya madai yao wanayodai kwa miaka 20 sasa.
Akizungumza kwa
niaba ya wenzake Mwenyekiti wa Kamati ya wafanyakazi hao Stumai Mohamed alisema
anashangazwa na kitendo cha Bodi ya Korosho kuwazungusha kwa muda mrefu kwa
kutowalipa fedha za mafao wanazodai toka mwaka 1997.
Alisema wengi
wa wafanyakazi hao walianza kazi mwaka 1988 hadi mwaka 1992 baadhi ya viwanda
vilibinafishwa na mashine zikauzwa. Wakaanza kudai fedha zao za mafao ili
ziwawezeshe kuwasomesha watoto na majukumu ya familia.
“Lakini
jambo la ajabu tunashangaa toka tuanze kudai walitulipa fedha kidogo yaani laki
moja na sabini tu kati ya milioni 9 tunazodai kila mmoja,”alisema.
Alisema kutokana
na Bodi hiyo kuwapa usumbufu walienda mahakamani katika mahakama ya kazi
kuishtaki Bodi hiyo na wakashinda kesi mwaka 1996 hivyo mahakama iliamuru
walipwe haki zao.
Bi. Mohamed
alisema kitu kingine cha ajabu ni kwamba bado wana barua za ajira na hadi sasa
hawajapewa notsi ya kuachishwa kazi hivyo gharama zinazidi kuongezeka.
Kwa upande
wake Mwanasheria wa Bodi hiyo Ugumba Kilasa alidai kuwa kwa vile hawana
wanachokijua kuhusu madai yao akawataka wapeleke kopi za hukumu ya kesi yao
inayoonyeshwa kwamba wanahitajika kulipwa mafao yao ili yaweze kufanyiwa kazi.
Hata hivyo,
pamoja na Mwanasheria huyo kujitahidi kujitetea kwa kila njia bado wafanyakazi
hao walidai kuwa leo hawataondoka katika Ofisi za Bodi hiyo na kwamba watalala
hapo hadi walipwe fedha zao.
No comments:
Post a Comment