Balozi wa Umoja wa Ulaya Filberto Sebregondi |
Umoja wa Ulaya umetoa Euro 2.5 sawa na shilingi bilioni 5 kwa ajili ya kusaidia sekta ya utamaduni na ubunifu nchini ambapo fedha hizo zimekabidhwa kwa serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Fedha na Uchumi.
Baada ya fedha hizo wadau mbalimbali wa viwanda vya ubunifu na utamaduni wameombwa kujitokeza kuchangia fursa hiyo. Watapewa fedha ikiwa tu wataweza kuandika proposal nzuri itakayowavutia waliotoa fedha hizo.
Balozi wa Umoja huo Filberto
Sebregondi alisema malengo ya mradi huo ni kutangaza na kuchangia sekta ya
utamaduni nchini kwa vile ni moja ya sekta zinazokua kwa kasi ambazo zinaweza
kusaidia kukuza uchumi wa nchi.
Alisema mradi huo umelenga katika
sehemu mbili ambapo ni kuhifadhi na kutangaza urithi na utamaduni na kujenga
uwezo dhidi ya ubunifu na utamaduni.
“Umoja wa Ulaya umelenga kusaidia
ubunifu na utamaduni hasa kutangaza na kukuza uwezo katika sekta hizo Tanzania,
na kwa kusaidia sekta hii itasaidia katika harakati za kupunguza
umaskini,”alisema.
Alisema mradi huo wa miaka mitatu
utasaidia kutangaza na kuwezesha mazingira mazuri ya ubunifu, ushirikiano na
kubadilishana uzoefu na vikundi mbalimbali katika shughuli za muziki, sanaa,
ubunifu, fasheni, filamu, video, uigizaji na picha na hivyo kuwainua kimaisha
na kusaidia kupunguza umaskini.
Pamoja na hayo, inakadiriwa kuwa mwaka 2010 mapato yaliyokusanywa kwenye sekta ya muziki
ilikuwa shilingi bilioni 222 lakini kutokana na kutotekelezwa kwa sheria ya
hati miliki ipasavyo serikali imekuwa ikipoteza mapato kiasi cha shilingi
bilioni 20 kutokana na sekta hiyo.
Ofisa Muidhinishaji wa mfuko wa
Maendeleo ya Ulaya kutoka Wizara ya
Fedha na Uchumi Samwel Marwa alisema
hayo jana kwenye mafunzo yaliyoandaliwa na
Umoja wa Ulaya kwa wadau wa viwanda vya ubunifu na utamaduni kujifunza
jinsi ya kuandaa mapendekezo yao kwa ajili ya kuomba za maendeleo ya sekta
hiyo.
Alisema kama sheria ya hati miliki
ingekuwa inatekelezwa vizuri wadau wa muziki
na pia serikali ingenufaika kwa kiasi kikubwa kwa kupata mapato mengi ambayo yangesaidia
kukuza uchumi wa nchi.
“Zipo fursa nzuri kupitia sekta hii
tatizo ni kwamba hata watu walioajiriwa katika muziki na sanaa kwa ujumla
hawajajiweka kibiashara, wanashindwa kuzilinda kazi zao hivyo zinaibwa ovyo kwa
hiyo kupitia mradi wa Umoja wa Ulaya wa kukuza utamaduni na ubunifu
tutarekebisha matatizo hayo,” alisema.
Alisema Umoja wa Ulaya tayari
umesaini Euro 2.5 sawa na shilingi
Bilioni tano na serikali ya Tanzania kwa ajili ya kusaidia sekta ya utamaduni
ili kuleta ubunifu mpya utakaowasaidia wahusika katika sekta na kuleta
mabadiliko yatakayosaidia pia serikali kukuza mapato yake.
No comments:
Post a Comment