TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Thursday 10 May 2012

Wadau msaidieni Kidunda aweze kwenda na nguvu mpya London


Makamu wa Rais wa Mchezo wa Ngumi za Ridhaa Tanzania Michael Changarawe kulia akikabidhi kombe katika moja ya matukio ya mchezo huo.
Makamu wa Rais wa Mchezo wa ngumi za Ridhaa Tanzania Michael Changarawe amesema baada ya Selemani Kidunda kuchaguliwa kushiriki mashindano ya Olympic yatakayofanyika London mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu ni jukumu la taifa kumtengenezea mazingira mazuri ya kumjenga.

Selemani Kidunda alikuwa ni miongoni wa wachezaji wanne wa ngumi wa Tanzania walioshiriki mashindano ya Afrika kufuzu kwenda Olympic nchini Uingereza yaliyofanyika nchini Cansablanca April 28 hadi Mei 7 ambapo alishindwa na mpinzani wake kutoka Morocco baada ya kushika nafasi ya tano. 

Hata hivyo, Kidunda   baadaye alijadiliwa na kuchaguliwa kuwa miongoni mwa watakaoenda kushiriki mashindano hayo ambapo kwa Afrika Mashariki ni wawili tu waliofuzu huku mmoja akitoka nchini Kenya.
Changarawe alisema Kidunda kabla hajaenda katika mashindano hayo ya kimataifa anatakiwa awekwe sehemu nzuri na kupewa chakula kitakachomjenga mwili ambapo anashauri  ni vema kambi yake ikawa na watu sita.

“Ili Kidunda aweze kuandaliwa vizuri kushiriki mashindano hayo naona kuna umuhimu katika kambi yake kuwe na  Makocha wawili mmoja wa ufundi na mmoja wa conditioning, daktari mmoja kwa ajili ya matibabu na wachezaji wengine wawili wenye uzito  kilo 75 na 69,”alisema Changarawe.

Naye mwalimu wa Kidunda ambaye alikuwa kwenye msafara huo Remmy Ngabo alisema kilichosababisha washindwe katika mashindano hayo ya Afrika  ni kutokuwa na mashindano ya kimataifa ya mara kwa mara.
Alisema Kidunda ni mchezaji mzuri hivyo anahitajika kuandaliwa mapema kwa maana ya kujengwa na kutafutiwa mazingira mazuri yatakayomwezesha kuipeperusha bendera ya Tanzania Kimataifa.

Kwa upande wake Selemani Kidunda alisema “nashukuru mashindano ya dunia niko peke yangu upande wa Tanzania, nilipigana sana sema tu waarabu walikuwa wanatoa pointi kwa kupeana lakini zaidi naomba watanzania waniunge mkono ili nijiandae vyema,”.


Awali, Kabla ya mchezaji huyo kuchaguliwa kwenda kushiriki mashindano ya Afrika kulikuwa na kambi tatu Tanzania za kuwachagua mabondia bora ambazo ni Jkt, Ngome na Magereza  na jumla ya mabondia 52 walijitokeza na 10 walichaguliwa na baadaye kutokana na ukosefu wa fedha walichaguliwa 4 ambao walikuwa ni Victor Njaiti, Abdallah Kassim, Selemani Kidunda na Amilian Patrick.


No comments:

Post a Comment