TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Monday 25 June 2012

Chanjo ya homa ya manjano kwa wasafiri


Na Mwandishi wetu

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inawajulisha wasafiri wote wenye umri zaidi ya mwaka mmoja wanatakiwa siku tisa kabla ya kuingia nchini Srilanka wawe wamepata chanzo ya homa ya manjano.

Kwa mujibu wa taarifa iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Regina Kikuli inaeleza kuwa utaratibu huo pia utahusisha wasafiri wanaopita nchini humo ambao watakuwa wanasubiri usafiri wa kwenda nchi nyingine.

Utaratibu huo umekuja kufuatia Wizara hiyo kupokea taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kuhusu chanjo ya homa ya manjano kwa wasafiri kutoka Tanzania kwenda Jamhuri ya Kisoshalisti ya Srilanka.

Kwa mujibu wa  Ubalozi wa Jamhuri ya Srilanka uliopo Afrika ya Kusini unaeleza kuwa kila msafiri anayeingia Srilanka atatakiwa kuwa na kadi ya chanjo ya homa ya manjano kama sharti la kiafya la kuingia nchini humo madhumuni makubwa yakiwa ni kudhibiti kuingia kwa ugonjwa wa homa ya manjano nchini humo.

Kwa wale wasafiri ambao hawatastahili kuchanja chanjo hiyo kutokana na sababu za msingi za kiafya kama vile wasafiri wenye umri chini ya mwaka mmoja, wazee wenye umri zaidi ya miaka 60, wajawazito, waathirika wa virusi vya ukimwi na wenye matatizo mengine ya kiafya watatakiwa kuonyesha uthibitisho kutoka kwa daktari.

No comments:

Post a Comment