TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Thursday 21 June 2012

Polisi Kenya kuwasaka walioua simba Nairobi


Polisi na mamlaka ya wanyama pori nchini Kenya wapo katika msako mkali kuwatafuta wakazi wa Kitengela walioua simba sita kutoka hifadhi ya taifa ya Nairobi.

Simba hao wanaodaiwa kuvamia na kuua kondoo 28 siku ya jumatono asubuhi.

Mkurugenzi wa huduma za wanyama pori Julius kipng’etih amedhibitisha mauaji hayo ya simba 6 na kondoo 28, na kusema Simba hao walipotea kutokea hifadhi ya Nairobi.

“nilazima tuwakamate waliohusika na mauaji haya ya Simba, wanapaswa kupambana na sheria” alisema mkurugenzi huyo.

Simba hao waliua ng’ombe 8 siku ya jumatatu, na hivyo wakazi wa eneo hilo kukosa uvumilivu baada ya Simba kuua tena kondoo siku ya jumatano.

Kwa  hisani ya swahilivilla

No comments:

Post a Comment