Polisi na mamlaka ya wanyama pori
nchini Kenya wapo katika msako mkali kuwatafuta wakazi wa Kitengela walioua
simba sita kutoka hifadhi ya taifa ya Nairobi.
Simba hao wanaodaiwa kuvamia na kuua
kondoo 28 siku ya jumatono asubuhi.
Mkurugenzi wa huduma za wanyama pori
Julius kipng’etih amedhibitisha mauaji hayo ya simba 6 na kondoo 28, na kusema
Simba hao walipotea kutokea hifadhi ya Nairobi.
“nilazima tuwakamate waliohusika na
mauaji haya ya Simba, wanapaswa kupambana na sheria” alisema mkurugenzi huyo.
Simba hao waliua ng’ombe 8 siku ya
jumatatu, na hivyo wakazi wa eneo hilo kukosa uvumilivu baada ya Simba kuua
tena kondoo siku ya jumatano.
Kwa hisani ya swahilivilla
No comments:
Post a Comment