Aliyekuwa Striker wa Chelsea Didier Drogba hatimaye amesaini
mkataba wa kuichezea club ya China Shanghai Shenhua kwa miaka miwili na nusu.
Mchezaji huyo atajiunga kucheza
katika timu hiyo ambapo ataungana na mchezji mwingine wa Kiafrika Nicolas
Anelka.
Drogba, mwenye umri wa miaka 34, alisema " Nilifikiria ofa zote
nilizozipata katika wiki chache zilizopita lakini Shaghai Shenshua ndio timu
niliyoichagua,”
Drogba anatarajiwa kucheza mchezo
wake wa kwanza akiwa na timu hiyo itakayochuana na Manster United Julai 25,
mwaka huu.
Drogba alijiunga Chelsea akitokea
Marseille kwa Euro 24m mwaka 200 |
No comments:
Post a Comment