Ben anasema
kwamba mama yake ni mwanamuziki wa siku nyingi na amekuwa akiimba nyimbo za
dini sema tu hajawahi kusikika wala kurekodi.
“Nataka kuja tofauti, na nitamshirikisha mama
yangu mzazi kwasababu ni mwimbaji mzuri wa muziki sema tu amekuwa akiimba zaidi
nyimbo za dini, naamini atafanya vizuri,”anasema Ben Paul.
Toka
ameingia THT tayari kwa mwaka huu amesharekodi nyimbo saba. Na ambazo zinavuma
sana kwenye vituo mbalimbali vya redio na Runinga ni pamoja na Samboira, my
number one na nyingine kibao.
Anawaleza
mashabiki wake kuwa kuna vitu vikali viko njiani hadi kufika mwishoni mwaka huu
atakuwa ametoa nyimbo nyingi nzuri hivyo wakae mkao wa kula kungojea mashairi
mazuri ya kuelimisha.
Msanii huyo
ni miongoni mwa wasanii waliopata tuzo ya Kilimanjaro Award katika wimbo wake
wa Samboira akiwa ni msanii bora anayeimba muziki wa taratibu kwa ladha inayowavutia wengi.
Mwanzoni
wakati Ben anaanza muziki alikuwa
akifanya kazi na Studio moja iliyokuwa ikijulikana kama Muziki Laboratory
ambapo ndipo alipotoa albam yake ya kwanza iliyokuwa ikijulikana kama
‘nikikupata’.
Wakati
anaanza muziki huo Ben alikiri kutonufaika mwanzo kwasababu alitegemea kuwa
angepata fedha za kutosha kwa ajili ya kuendelea na masomo yake ya Chuo Kikuu.Lakini kwa sasa anajivunia mafanikio baada ya kujiunga na Jumba la Sanaa (THT) kwa vile anaweza kupata shoo nyingi zinazomlipa. Kwa sasa ameweza kujiunga Chuo cha Usimamizi wa Fedha(IFM) ambapo anachukua masomo ya Benki.
No comments:
Post a Comment