Na mwandishi wetu
MFANYABIASHARA
Adam Karista (21) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala
akikabiliwa na mashitaka ya kutumia kisu kuiba mali zenye thamani ya Sh Sh
800,000.
Karista
alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Ester
Mwakalinga.
Wakili wa
Serikali Naima Mwanga alidai kuwa, Desemba 9 mwaka jana katika eneo la Buguruni
Kisiwani, Karista na wenzake ambao bado hawajafikishwa mahakamani walipanga
njama na kuiba mali mbalimbali zenye thamani hiyo.
Naima aliendelea
kudai kuwa, kabla ya kuiba mali hizo , Karista alitumia panga kumtishia John
ili achukue mali hizo bila kipingamizi.
Mshitakiwa
alikana mashitaka na kurudishwa rumande kwa kuwa kesi ya unyang’anyi wa kutumia
silaha haina dhamana.
Katika hatua
nyingine, Mohamed Abas (40) amefikishwa katika Mahakama hiyo kwa tuhuma za
kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Wakili wa
Serikali Aidah Kisumo alidai mbele ya Hakimu Tarsila Kisoka kuwa Aprili 28
mwaka huu saa 5:00 katika mtaa wa Uhuru, Abas alijipatia Sh milioni 12 kutoka
kwa Kunambi Hamisi kwa madai ya kumrudia lakini hakufanya hivyo.
Mshitakiwa
alikana shitaka na kurudishwa rumande hadi Juni 28 mwaka huu kesi hiyo
itakapotajwa tena.
No comments:
Post a Comment