Na Mwandishi wetu
MKAZI wa Mbagala aliyetambulika kwa jina moja la
Shaibu (35) amekutwa amekufa chumbani kwake baada ya kunywa sumu ya panya.
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Temeke David Misime alisema kuwa, tukio hilo lilitokea
juzi jioni katika eneo la Mbagala baada ya polisi kukutwa mwili wa marehemu.
Alisema kuwa
maiti hiyo ilikutwa imelala chumbani kwake ikiwa haina jeraha sehemu yoyote
huku kukiwa na matapishi pembeni.
Misime alisema,
uchunguzi wa awali umebaini kuwa marehemu alikunywa sumu ya panya
na chanzo cha kujiua hakijafahamika kwasababu marehemu hakuacha ujumbe wowote
Alisema mwili
wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke kwaajili ya uchunguzi
zaidi.
Katika hatua
nyingine, mkazi wa Boko, Salum Said (19) amekufa baada ya kuzidiwa na maji
wakati akiogelea katika ufukwe wa bahari ya Hindi.
Misime alisema, tukio hilo lilitokea juzi mchana wakati Said akiwa anaogelea
na mwili wake uliopolewa na Askari wa zima moto wakishirikiana na Askari polisi na umehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke .
Misime alisema, tukio hilo lilitokea juzi mchana wakati Said akiwa anaogelea
na mwili wake uliopolewa na Askari wa zima moto wakishirikiana na Askari polisi na umehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke .
Wakati huo
huo, mtembea kwa miguu asiye fahamika jina alikufa papo hapo baada ya kugongwa na gari
katika barabara ya Mandela.
Kamanda wa
polisi Mkoa wa Kinondoni Charles Kenyela alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi
mchana na kuhusisha gari aina ya Toyota Rav4 yanye namba T568 AVL .
Alisema gari
hilo lilikuwa likiendeshwa na Fadhili Kazia (35) likitoka maeneo ya
buguruni kwenda Ubungo lilimgonga
mtembea kwa miguu na alikufa papo hapo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika
hospitali ya Amana
No comments:
Post a Comment