Mbunge
wa jimbo la Singida mjini Mohammed Gullam Dewji, ametumia zaidi ya shilingi
milioni 22 kugharamia uchimbaji wa kisima kirefu cha maji cha kitongoji cha
Mtisi, kata ya Mtamaa.
Dewji
ambaye pia ni mjumbe wa NEC mkoa wa Singida, akizungumza wakati wa hafla ya
uzinduzi wa kisima hicho, Alisema fedha hizo zimetumika pamoja na mambo mengine
katika utafiti wa eneo lenye maji,uchimbaji na ununuzi wa pampu ya mkono.
“Hapa
naomba niweke mambo wazi, gharama hii inajumuisha pia uchimbaji wa kisima
ambacho kwa bahati mbaya baada ya uchimba kina kirefu sana,kikawa hakina
maji. Pamoja na kukosekana huko kwa maji, lakini fedha nyingi
zilitumika”,alifafanua.
Dewji
alisema ameamua kutumia fedha zake binafsi kugharamia uchimbaji huo wa kisima,
kwa lengo la kuwapatia maji safi na salama wakazi wa kata ya Mtamaa.
“Mimi
binafsi naamini kwamba maji safi na salama, yatasaidia kuondoa uwezekano wa
kutokea kwa magonjwa ya mlipuko ikiwemo, ugonjwa wa kuharaa”,alisema.
Aidha,
mbunge huyo aliwataka wakazi wa kijiji cha Mtamaa na vijiji jirani, kukitunza
kisima hicho ili kiweze kutoa huduma endelevu.
Dewji
alisema kazi ya uchimbaji wa visima, ni ya gharama kubwa mno, hivyo ni
muhimu kisima hicho kikatuzwa vizuri na kila mkazi wa eneo hilo, awe
mlinzi ili kisiharibiwe.
Awali
diwani wa kata ya Mtamaa (CCM) Mbua Chima, alitumia fursa hiyo kumshukuru
mbunge Dewji, kwa msaada wa kuwachimbia kisima wakazi wa kata hiyo.
Kwa hisani ya Mo blogu
No comments:
Post a Comment